Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Lindi,Abdulaziz Ahmeid (Channel ten) akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa ,Reubern Mfune kufungua mafunzo ya siku nne kwa wanahabari hao.
Mwezeshaji wa Mafunzo hayo Bw Juma Thomas,Mwanasheria wa kujitegemea akitoa mafunzo kwa wanahabari.
Wanahabari toka vyombo mbalimbali wakihudhuria mafunzo hayo ili kujengewa uwezo wa kuandika kwa mujibu wa sheria Habari za mahakamani.
Wanahabari wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Lindi wakiwa katika Picha ya Pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Bw Reubern Mfune mara baada ya kufungua mafunzo ya siku nne kwa ya kuwajengea uwezo wanahabari... kuhusiana na uandishi wa Habari za Mahakamani. 

Wanahabari 18 wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Lindi kufuatia mradi wa "Press club" Wameanza mafunzo ya uandishi wa habari za mahakamani ikiwa ni mfululizo wa Mafunzo yanayoendeshwa na Umoja wa Vilabu vya waandishi wa Tanzania.

Mafunzo hayo ya siku nne yanayoshirikisha wanahabari toka vyombo mbalimbali yameanza jana Wilayani Ruangwa na kufunguliwa na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo.

Baada ya mafunzo hayo Wanahabari hao watafanya mkutano mkuu wa mwaka wa klabu hiyo ikifuatiwa na Mkutano wa Wadau wa Habari walio katika wilaya hiyo Mafunzo hayo yanayoendeshwa kwa ufadhili wa mradi wa Press Club Chini ya Umoja wa Vilabu vya waandishi wa habari Tanzani(UTPC)Yameanza leo wilayani Ruangwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...