Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar wakiwa wanasubiri treni ya mwakyembe iwasili stesheni ikitokea ubungo maziwa tayari kwa safari ya kuwarudisha Majumbani Kwao. Baadhi ya Abiria wakiwa wamewahi kwaajili ya Kupanga foleni ili waweze kupata siti huku wengine wakichuchumaa kutokana na kulisubiri kwa muda
 Abiria Wakiteremka katika treni linalofanya safari zake ndani ya Jiji la Dar mara lilipowasili Katika Kituo cha Stesheni karibu na central polisi tayari kwa safari ya kurudi tena Ubungo
Baadhi ya Abiria waliogeuza na treni hilo wakiwa wamepandia Kituo cha Kamata Ili kuwahi Siti ambapo walipelekea sintofahamu kwa baadhi ya abiria waliokuwa kituoni hapo na kutaka kupanda kwenye hilo behewa kukuta likiwa tayari limeshajaa kutoka na abiria kugeuza na treni hilo wakati utaratibu huwa haurusiwi na ikifika mwisho abiria wote wanatakiwa kushuka
 
Abiria wakianza kupanda treni tayari kwa kurejea makwao mara baada ya treni la mwakyembe kuwasili kituoni hapo kwenye majira ya saa kumi na moja na dakika ishirini jana
 Mmoja wa Abiria aliyegeuza na treni hilo ambapo walipandia Kamata kwa lengo la kuwahi kiti akibishana na mmoja katika ya abiria ambao walikua kwenye foleni muda mrefu wakisubiria treni hilo kufika ili waweze kuingia ndani na kupata siti ambapo alikuta behewa hilo likiwa limeshajaa na kuanza kubishana huku abiria waliokuwa wakisubiri treni hilo wakitaka abiria waliogeuza na treni hilo kushuka
Wakazi wa Jiji la Dar wakiwa kwenye foleni ya kupanda treni maarufu kwa jina la treni ya mwakyembe jana kwenye majira ya saa 11 jioni katika kituo cha Stesheni tayari kwa kurudi nalo ubungo huku baadhi ya behewa kuwa limeshajaa kabla hata halijafika kituoni hapo kutokana na abiria kugeuza nalo kwa lengo la kuwahi siti. Behewa ambalo lilikuja likiwa limeshajaa ni behewa lenye namba 3644 ambalo abiria wake walikua wamepandia njiani kwa nia ya kugeuza nalo ili waweze kupata siti.
Wakazi wa jiji la Dar wakipanda kwenye treni la mwakyembe mara baada ya kuwasili kwenye kituo chake cha Stesheni jana Kwenye majira ya Saa 11 Jioni jana tayari kwa kuwarudisha majumbani kwao likitokea Mjini kuelekea Ubungo ambapo ndio kituo cha Mwisho

Na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

Katika hali isiyo ya kawaida jana kwenye majira ya Saa 11: 20 Jioni katika kituo cha Treni kilichopo stesheni mkabala na Kituo Cha Polisi Cha Cetral kuliibuka Jambo la kushangaza wakati abiria wanaosubiria treni inayofanya kazi zake ndani ya jiji la dar kuona behewa moja likiwa limeshajaa tayari kutokana na abiria kupandia njiani na kugeuza nalo kwa lengo la kuwahi siti na kupelekea abiria waliowahi kituoni hapo na  kupanga foleni kwaajili ya kuwahi siti kuambulia patupu.

Abiria waliokuwa wakisubiria treni hilo walianza kulalamika pale ambapo walikuta behewa hilo limeshajaa kabla hata treni hiyo haijafika kwenye kituo chake cha mwisho kwa lengo la abiria hao kuwahi . 

Baada ya Tukio hilo kutokea kulizuka sintofahamu kwa baadhi ya wafanyakazi na Askari Polisi ambao hawajawahi kuona utaratibu huo ukifanyika na kupelekea Abiria kuhisi tayari wafanyakazi wa treni hiyo waneshaanza kuchakua kitu ambacho utaratibu hauruhusu. 

Utaratibu uliopo ni kwamba hata kama abiria amepandia katikati anatakiwa kuteremka pindi treni hilo linapofika mwisho wa kituo ndipo akate tiketi kwaajili ya kupanda tena na kurudi nalo lakini hali imekuwa tofauti hapo jana baada ya abiria hao kutokushuka na tiketi kukatiwa ndani na kupelekea abiria waliokuwa wakisubiri treni hilo kusubiri kwa muda mrefu.

Lukaza blog imeweza kunakili sauti za abiria ambao waliokuwa wakilalamika juu ya utaratibu huo uliofanywa na wafanyakazi ambao sio waaminifu na kupelekea usumbufu kwa abiria ambao wamewahi kupanga foleni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. aibu kubwa sana kweli bongo bado tupo nyumba miaka 100, hivi kweli tokea lini train likatumia mlango mmoja tu kwajili ya kupandia abiria na kushukia?

    na hivi inashindikana vipi kuweka ukuta au kijukwaa cha kushukia train au kupandia ? watu wanashuka na kupanda ngazi za train ni hatari sana wanaweza kusababisha kuvunja kwa miguu

    hivi watu wazima wanawezaje kupanda hilo train?

    mnatuaibisha sana serikali baada ya kututoa kimaso mnatupakazia kuwa na train za ajabu kama hizo huduma mbovu foleni utasema sukari enzi za nyerere

    aibu aibu aibu kubwa.

    ReplyDelete
  2. Usafiri wa Mjini kwa Treni,

    Ni usafiri wa Halaiki, hivyo msitegemee kuwa lazima abiria upate kiti!

    Huu ni usafiri wa kuwa tayari kwa kusimama ikibidi, acheni mipango yenu mibovu ya kwenye Mabasi ya kugeuza nalo kama mnavyo fanya asubuhi: MkIwepo,

    -Ukonga Banana na Ukonga Mombasa kugeuza nalo Gongolamboto kurudi na basi Posta.

    -Kimara Baruti na Kimara Bonyokwa, kwenda Kimara mwisho na Kurudi na basi Posta

    -Mbagala Zakhem kugeuza na basi Mbagala Rangi 3 na kurudi na basi Posta.

    Mjaribu kubadilika na kuukubali mpango mpya wa usafiri kwa manufaa ya wengi!!!

    ReplyDelete
  3. Huo ni ubwege mtozeni kwa nini mgeuze na mabasi kama Mataahira?

    ReplyDelete
  4. Huo ni ubwege mtozeni kwa nini mgeuze na mabasi kama Mataahira?

    ReplyDelete
  5. Kama mmesha anza kugeuza na Treni ya MWAKYEMBE ni moja kwa moja, hata katika Mpango wa Mabasi yaendayo kasi ya MAGUFULI mtakuwa mnageuza nayo!!!

    ReplyDelete
  6. Watanzania tustaarabike.hii itasaidia kuwapa moyo viongozi wetu kuendelea kuleta maendeleo.TUBADILIKE!!

    ReplyDelete
  7. Angalieni Wabongo hawa!

    Sasa wajameni hizi Treni ni za safari za Mjini mnageuza nayo wakati safari yenyewe inachukua sio zaidi ya saa 1 au chini ya Dakika 60, kwani mkae kwenye viti mnakwenda Tabora au Kigoma?

    ReplyDelete
  8. Nadhani kwa kuwa nia ya watoa huduma ni kutoa huduma iliyo bora nadhani kwa upande mwingine nauli ya mtu anayegeuza na gari moshi iwe mara tatu ili kuchuja mzunguko huo. ER

    ReplyDelete
  9. Da kazi kweli kweli, halafu unaambiwa Bongo tambarale.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...