Ofisa wa utendaji na Mafunzo wa Jeshi la Wanamaji wa Tanzanai Brigedia Jenerali Abdallah Athuman Mwemnjudi (kushoto) akitoa maelezo leo jijini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa zoezi liitwalo Cutlass Express 2 linaloshirikisha wanamaji kutoka Marekani, Msumbiji, Netherland na Tanzania likiwa na lengo la kubadilishana uzoefu na mawazo juu ya kupambana na uharamia katika mwambao wa Bahari ya Hindi. Kulia ni Kiongozi wa Kundi namba 1 la wanamaji wa NATO Commodore Ben Bekkering.
Kiongozi wa wa Kundi namba 1 la wanamaji wa NATO Commodore Ben Bekkering (kulia) akijibu maswali ya waandishi wa habari mjini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa zoezi liitwalo Cutlass Express 2 linaloshirikisha wanamaji kutoka Marekani, Msumbiji, Netherland na Tanzania likiwa na lengo la kubadilishana uzoefu na mawazo juu ya kupambana na uharamia katika mwambao wa Bahari ya Hindi. Kushoto ni Ofisa wa utendaji na Mafunzo wa Jeshi la Wanamaji wa Tanzanai Brigedia Jenerali Abdallah Athuman Mwemnjudi.



mwenye kuyaweza maji hapo ni huyo muholanzi tu hapo ...hizo nchi nyengine munaongeza idadi tu, hao wadachi nilipita kwao hivi karibuni kila kona kuna maji nchi mzima ni maji matupu mutafaidika nao kwa mengi kwa masuala ya maji ni kweli wataalamu mukichukuliwa kwao munaweza kujifunza mengi sana kama hamtakimbia darasani mukafuatilia VIOO kwani na utaalamu huo wako nao
ReplyDelete