Mshindi wa jumla wa mashindano ya kuwania kombe la Johnnie Walker Waitara 2012 Sudson Manatsa akinyanyua juu vikombe vyake viwili alivyoshinda wakati wa Mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gofu Lugalo jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalidhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake kikali cha Johnnie Walker.
Mgeni rasimi wa Mashindano ya Johnnie Walker Waitara Trophy,  Mlezi wa Gofu nchini Kenya na Mkurugenzi wa ICEA LION, Dunkan Nderitu Ndengwa kutoka nchini Kenya  akimkabidhi zawadi Mshindi wa jumla wa mashindano ya kuwania kombe la Johnnie Walker Waitara 2012 Sudson Manatsa. Kampuni ya Bia ya Serengeti imedhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Johnnie Walker.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Stephen Gannon  akimkabidhi zawadi Mshindi wa pili wa  daraja A, Aidan Nziku  kikombe na zawadi nyingine baada ya kuibuka mshindi wa kundi hilo katika mashindano ya kuwania kombe la Johnnie Walker Waitara 2012. Kampuni ya Bia ya Serengeti imedhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Johnnie Walker.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...