MWENYEKITI WA MTAA HUO HABIBA MWAKITALU AMEMBEBA MTOTO ANETH TAYARI KWA KUMPELEKA HOSPITALI HUKU NYUMA AKIFUATIWA NA MWESHIMIWA DIWANI KATA YA MAJENGO SAMWELI


WANANCHI WENYE HASIRA KALI WALIMCHUKUA MAMA HUYO NA KUMPELEKA KITUO CHA POLISI


MTUHUMIWA NA MGONJWA WANAINGIZWA KATIKA GARI LA MWESHIMIWA DIWANI TAYARI KWA KUPELEKWA POLISI
PICHA Na  KALULUNGA,
HABARI na  EMANUEL MADAFA

Mkazi wa kitongoji cha Majengo jijini Mbeya Ndugu Bahati Rukangara amemchoma moto mtoto mdogo wa miaka 3  kisha kumfungia Ndani na kumlazimisha ale kinyesi chake.

Mwenyekiti wa mtaa huo Ndugu Habiba Mwakitabu amesema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa 10 :30 asubuhi ambapo majirani na mwanamke huyo waligundua mara baada ya kusikia sauti ya mtoto huyo akilia kutokana na maumivu.

Amesema mara baada ya kusikia sauti hiyo walifika eno hilo na kunza kumhoji ili kufahamu kiini cha tatizo hilo ambapo alishindwa kutoa ushirikiano. Majirani walilazimika kubomoa mlango ndipo walipomkuta mtoto huyo akiwa uchi huku ameungua vibaya mwilini hasa upande mmoja wa  mkono wa kushoto .

Amesema mara baada ya kumhoji mtoto huyo aliwaeleza kuwa mama yake mdogo alichukua nguo na kumfunga mkononi kisha kumwagia maji ya moto pamoja na kumlazimisha ale kinyesi chake hali ambayo iliwafanya washindwe kuvumilia na kuanza kupiga kelele kwa lengo la kuomba msaada kwa watu wengine.

Kwa mujibu maelezo ya mwenyekiti huyo amesema kuwa Mtuhumiwa huyo amekuwa akifanya vitendo vya manyanyaso kwa mtoto huyo mara kwa mara ambapo wamekuwa wakimuonya lakini amekuwa si mtu wa kusikia.
Amesema mtoto huyo si wa kwa kwakwe kwani amekuwa akiishi naye kwa muda mrefu sasa ambapo aliachiwa na dada yake ambaye hafifahamiki aliko kwa sasa.

Diwani wa kata hiyo Ndugu Samuel Mamboma alifika eneo hilo tukio na kutoa msaada wa usafiri kwa lengo la kumfikisha mama huyo polisi pamoja na mtoto huyo ambaye naye alikimbizwa Hospitali.
Hata hivyo amesema tukio hilo si la kwanza kutokea katika meaeno hayo kwani kumekuwepo na matukio mengi hasa ya utoaji mimba na kutupwa watoto.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Huu ni unyama wa hali ya juu, yaani unafanya ukatili kama huu kwa mtoto ambaye hajui hata alitendalo masikini. ivi amekosa nini huyu mtoto mpaka umpe adhabu kali ya kula kinyesi na kumchoma moto? Hongera kwa majerani ambao waliamua kubomoa mlango ili kumuokoa mtoto nadhani ingekua mbaya zaidi kwa mtoto iwapo kusingekuwepo watu karibu. Nipo ulaya huu ni mwaka wa nane hakuna upendo kama huo ulioneshwa na hao majerani kwa kudiriki hata kuvunja mlango, huku jeerani humjui hakujui likitokea la kutokea ni la kwako peke yako. Hongera watanzania kwa kudumisha upendo na mshikamano.

    ReplyDelete
  2. Pole sana mtoto. Nimeumia sana, kama baba wa binti wa miaka mitatu. Ninakuombea upone na pengine kwa vile si rahisi urudi tena kwa huyu mama anayekutesa, basi Mungu akuweke kwenye mikono ya watu wanye upendo na kujali ili ukue vizuri kama watoto wengine. Nawashukuru saaana majirani kwa moyo wenu wa upendo na kujali. Kwa kweli watanzania pamoja na uswahili wetu, bado roho ya upendo tunayo. Mbarikiwe saaaaana!

    ReplyDelete
  3. wewe au wa kwanza jiangalie wewe kama haujui majirani, navyojua mie wazungu ni wambea kupita hawawezi kaa kimya wakisikia kelele za watoto za kushtua kama hivi.

    mnapenda sema watu wana rohom
    mbaya mbona hata Dar hapo majirani hawajuani hata kuzoeana kama zamani, imeanza wengi kila mtu na lake. hata watoto wanaojumuisha wazazi kujuana hawaonekani mitaana sana maeneo mengi wakicheza wote.

    na nyie au wewe kuwa unasalimia sio wote roho mbaya as sie tunayo roho mbya hta ya kutesa wafanyakazi. sasa ukianza kuwaonyesha una utu utaona usipojiachia ukawa mwoga nao wanakupotezea wakizani haupendikujuana.

    il ya kelele, ugomvi kusemewa na hao hao majirani ni namba moja. wanapiga polisi mambo mbele.

    ReplyDelete
  4. Wewe sema ilivyo usiseme ulipo.ulaya ulaya ndio nini Sasa Wewe mshamba wa ulaya? vipi Wewe

    ReplyDelete
  5. Haya, na huyo mama ni msomali?

    ReplyDelete
  6. mi nazani huyu dada anamatatizo ya akili kwani mtoto wa miaka mitatu anajua nini niliposoma hii nilimwangalia mwanangu ambaye anamiaka mitatu, nikaona huyu akapimwe akili?mtoto bado ni mdogo sana huyo ajui hata kula mwenyewe, au ajazaaa heeeeeee.

    ReplyDelete
  7. Huyo mwanamke lazima atakuwa mchawi na ameshakula nyama ya mtu kama alivyosema nyerere, na afichwe asionekane tena duniani maana kizani chake kibaya hakitakiwa duniani.

    ReplyDelete
  8. POLE SANA MTOTO. MWENYEZI MUNGU NDIYE MUWEZA WA YOTE, AKUPONYE NA KUKUPA AFYA NJEMA.

    Yaani nimesikitika sana huyo mama mdogo mlivyomshika kwa kumbembeleza, angekuwa huku kwetu kwa kweli angejuta kuzaliwa. Maana akepata kipigo cha mbwa mwizi, walau na yeye auguze vidonda. Angefika polisi akiwa atamaniki, uso hasomeki.

    ReplyDelete
  9. Haya Sasa tungependa kujua kama na Huyo mama Ni msomali? Pole sana mtoto Mungu atakusaidia na Huyo mama lazima apelekwe mbele ya haki. Majirani hongera sana Kwa kazi mliyo fanya neibour watch Ni asili yetu wa bongo big credit to them majirani. Michuzi tafadhali to feedback mwisho wa kesi hiii

    ReplyDelete
  10. WEWE Mwanamke unyama uliomfanyia mtoto unastahili kunyang'anywa mtoto na wewe kufungwa Gerezani.

    Kama ulizaa na hutaki kumlea mtoto kwa kumdhalilisha na kumtesa kwa nini kama umeshindwa usimkabidhi mtoto kwa wengine alelewe?

    Huyo mtoto sio wako pekee bali ni rasilimali ya nchi na wananchi kwa ujumla licha ya kuwa umemzaa wewe.

    Unajuaje?, inawezekana unatutesea Raisi wetu wa baadae na sisi wa Tanzania hatuwezi kukubali kwa hilo!

    ReplyDelete
  11. Wabeba boxi utawajua kwa maandishi yao. Full frustration, full povu

    ReplyDelete
  12. Huu ukatili si wa kawaida. Huenda ana schizophrenia huyo dada. Anatakiwa apate huduma ya hospitali huyo. Mama na baba wa mtoto nao punguwani. Watamwachiaje mtoto wa miaka 3 mtu mwingine. Enyi wazazi, tukumbuke wajibu wetu kwa watoto.Tumewaleta wenyewe duniani ni jukumu letu sisi wenyewe midhali tuko wazima kuwalea na kuwalinda.

    Hongera kwenu majirani wa huyo katili, wameonyesha utu wa hali ya juu. Wamekuwa mfano wa kuigwa kwa jamii kwa kutovumilia hali hii. Ukweli hii social structure ya nyumbani ni katika mambo ambayo tunaya-miss tulioko ughaibuni.

    ReplyDelete
  13. huyo mama afanyiwe kama alivyo mfanyia mtoto ili aone uchungu kama huyo mtoto alivyo uona. huwezi kukaa na mtoto si umpeleke sehemu atakayopata msaada kweli mtoto wa miaka mitatu kweli???? anajua nini jamani laiti ningekuwa hapo sijui huyo mama ningemfanya nini naomba vyombo vya habari vifuatilie kwa kina na haki za binaadamu sijui wako wapi jamani.

    ReplyDelete
  14. Kwa kweli nimeumia sana. Pole sana Aneth. Nafahamu machungu uliyoyapata. Kumbuka hata ukimwagiwa kikombe cha chai jinsi mtu unavyoumia sembuse kumwagiwa maji kwa mtindo huo?. Niseme kuwa kama mtu huwezi kumtunza mtoto wa mwenzio huna haja ya kujifanya unaweza kumtunza wakati roho yako ni mbaya au ina mtima nyongo. Akina baba mnaozaa nje ya ndoa na kukusanya watoto kuwapelekea wake zenu kwa mabavu hata kwa hiari kumbukeni haya ndio yanayowapata. Anaweza asimwagiwe maji lakini akapewa vijineno vidogo vidogo vikamfanya asiishi kwa raha na baba ukiarifiwa unakuja mbogo kwa huyo mtoto bila ya kufanya utafiti. Kumbukeni mtoto anayelelewa na mtu ambaye sio mama yake mzazi huwa hawana uhusiano wa karibu kwa kuwa kibaolojia hawana damu ya pamoja. Fungukeni jamani. Nina imani vyombo vya dola vitafanya kazi yake na sheria kuchukua mkondo wake ili adhabu kali itolewe kwa huyu binti ili kuwa fundisho kwa watu wengine wenye tabia ya aina hii.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...