Unapotaja majina ya wapiganaji wakongwe kisiwani Zanzibar hutokosa kutaja jina la Farouq Karim wa ITV ambaye toka asubuhi utasikia sauti yake ikipasha haya na yale karibu kila siku ya Mungu kwa miaka inakaribia 15 sasa. Faroq, ambaye jina lake la utani ni Zinadine Zidane 'Zizzu', amezaliwa na kukulia katika habari ambapo baba yake Mzee Karim (RIP) ndiye wakala mkuu wa magazeti Zanzibar toka enzi hizo katika duka lao la Masomo Bookshop, nyuma ya Markiti mitaa ya Shangani. Kazi hiyo ameirithi uzuri  tu na anaendeleza Libeneke kama anavyoonekana katika taswira hizi
 Hapa ni hesabu kwa kwenda mbele
Wadau wakipitia vichwa vya habari Masomo Bookshop, Zanzibar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hawa watu wenye tabia ya kusomea magazeti ukutani au mezani wanaharibu biashara za wenzio. Unakuta mtu kasimama anasoma habari zote kisha anaondoka hanunui. Hivi ni tabia gani hii?
    Mdau, CA USA

    ReplyDelete
  2. marikiti nyuma shangani ndio vipi mbona unatuchanganya?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...