LIGI Kuu ya Tanzania bara mzunguko wa pili ipo kwenye hati hati ya kutofanyika baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuzifungia akanti za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na TFF kudaiwa zaidi ya milioni 100 na TRA. 

 Hatua hiyo ya TRA ya kuzifungia akaunti hizo za TFF, imekuja baada ya TFF kukiuka taratibu za kuwakatia kodi makocha wa kigeni wanaozifundisha timu za Taifa tangu kipindi cha Mbrazil Marcio Maximo. 

Akizungumza kwenye ukumbi wa hostel za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Kaimu katibu mkuu wa shirikisho hilo ambaye pia ni mkurugenzi wa ufundi, Sunday Kayuni alisema kutokana na hatua ya TRA kuzifungia akaunti hizo huenda Ligi Kuu mzunguko wa pili isifanyike kutokana moja ya akaunti hizo kuwa na zaidi ya Sh.350m za klabu ambazo zimetoka katika kampuni ya Vodacom ambayo ndiyo mdhamini wa ligi hiyo.

 "Akaunti zetu zote zimesimamishwa na TRA kwa kile kilichodaiwa kuwa hatujalipa zaidi ya sh 100 milioni za kodi za mishahara ya makocha wote waliowahi kuzifundisha timu za taifa kuanzia kipindi cha Maximo hadi Sasa."alisema Kayuni ".

Kufatia hali hiyo kunauwezekano mkubwa wa Ligi Kuu mzunguko wa pili kutofanyika kwa sababu moja ya akaunti hizo ilikuwa na zaidi ya sh 350 za klabu kutoka Kampuni ya Vodacam wadhamini wakuu "Wote tunafahamu kuwa hali halisi ya klabu zetu kiuchumi hivyo kufungiwa kwa akaunti hizo kutaathiri moja kwa moja mchakato mzima wa ligi kwani timu nyingi zinategemea fedha hizo kwa mambo mengi ikiwa ni pamoja na maandalizi ya ligi" alisema Alisema.

  TRA kufungia akaunti za TFF, imekiuka taratibu za kodi kwani shrikisho hilo halipaswi kulipa kodi hiyo kwa sababu siyo linalolipa mishahara ya makocha hao. Alisema Kodi hiyo ilipaswa kulipwa na Serikari ambayo ndiyo inayolipa mishahra ya makocha hao na siyo TFF.

 "Hakika hatujatendewa haki na huu ni uonevu, hatahivyo pia tumejaribu kufuatilia lakini tumekuwa tukipigwa danadana....."

Pia tunasikitika Serikali kupitia Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo haionyeshi ushirikiano juu ya jambo hili ambalo linatufanya tuone kuwa kuna kitu hapo katikati," alisema Kayuni ambaye alikuwa samabamba na Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Said Mohamed pamoja na Mtendaji Silas Mwakibinga. 

Katika hatua nyingi Kayuni alisema kuwa wapo kwenye mchakao wa kuunda kamati maalum itakayohusisha TFF pamoja na wawakilishi wa klabu ili iweze kukutana na TRA kwa mara nyingine tena kuangalia uwezekano wa kutatua tatizo hilo. 

Hata hivyo Kayuni alisisitiza kuwa TFF haitalipa kodi hizo na haina fedha za kulipa sababu siyo inayotakiwa kufanya hivyo kwa mijibu wa sheria ya kodi sababu siyo inayolipa mishahara ya makocha hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...