Ndege iliyokuwa imembeba Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda ikiwasili katika uwanja wa ndege wa Mjini Mpanda mapema hii leo. Waziri Mkuu atakuwa Wilayani Mpanda kwa shughuli kuu mbili ambayo moja ni kikao cha tathmini ya kongamano la uwekezaji lililofanyika wilayani hapa Oktoba mwaka jana pamoja na uzinduzi wa Mkoa mpya wa Katavi ambapo Mgeni rasmi atakuwa Mhe. Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal na kilele itakuwa siku ya jumapili tarehe 25/11/2012.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Col. Mst. Issa Machibya mara baada ya kuwaisili katika uwanja wa ndege wa Mjini Mpanda mapema hivi leo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda aikipokea maelezo kuhusu uwekezaji kutoka kwa Muwezeshaji katika banda la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa Bwana Misasi Nyanda Marco ambaye pia ni Afisa katika dawati la uwekezaji.
Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Mhandisi Emmanuel Kalobelo akifurahia jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwezeshaji na Uwekezaji Mhe. Marry Nagu wakati wa mapokezi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda leo katika uwanja wa ndege wa mjini Mpanda.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Iddi Hassan Kimanta akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwezeshaji na Uwekezaji Mhe. Marry Nagu mapema leo asubuhi kwenye mapokezi ya Mhe. Waziri Mkuu katika uwanja wa ndege wa Wilayani Mpanda.Picha na Hamza Temba,Katavi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ankal swali la kizushi kwako la kukupatia usingizi...Siku hizi naona kama kuna Camera zikipiga ndege kama hiyo inayotembea na pangaboya zinazunguka,picha inatoka kama pangaboya zilivyokuwa yaani unaona kwamba pangaboya zilikuwa zinazunguka(Ni kweli zipo au ni photo editor? au setting ya Camera?),na kuna Camera kama hii iliyotumika hapa Pangaboya zinaonekana zimetulia.Ndiyo,kwenye fizikia tuliambiwa pangaboya zinatakiwa zionekane zimetulia,mambo ya mwendo wa mwanga wa Kamera n.k.Lakini naona kama siku hizi hiyo 'law' inapitwa na wakati.Karibu Ankal

    David V

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...