Meneja wa Tanesco mkoa wa
Temeke Eng. Richard Malamia akiwa na ofisa Mipango wake Bi. Cecilia Msangi
wakiangalia nguzo ambayo haina sifa ya kusambazia umeme ambayo inasadikiwa
imewekwa na vishoka katika maeneo ya Mbagala, Chamazi kwa Musoma jijini Dar es
salaam leo. Eng. Malamia alifanya ukaguzi wa kustukiza katika maeneo hayo akishirikiana na watalamu
wake baada ya kupokea malalamiko ya kuwepo
kwa upungufu wa umeme katika maeneo hayo. Baada ya kufanya ukaguzi alibaini kuwepo na watu waliojiunganishia
umeme visivyo halali kupitia nguzo hiyo. Chini akiongea na baadhi ya wakaazi wa eneo hilo akiwa na wasaidizi wake. Picha na Chris Mfinanga
Home
Unlabelled
Nguzo ya umeme ya magumashi yabambwa Mbagala
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Jamani ifike mahali tuwajue hao vishoka ni akina nani kama si kikulacho!!?
ReplyDelete