Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)  Bi. Irene Isaka akiwasilisha  maada kuhusiana na sekta ya Hifadhi ya Jamii  Tanzania. Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii  (SSRA ), leo  hii imeendesha  semina kwa Wafanyakazi  Wa Bodi ya Mishahara  na Maslahi Katika Utumishi wa Umma. Semina hiyo imelenga katika kuelimisha wafanyakazi  Wa Bodi ya Mishahara  na Maslahi Katika Utumishi wa Umma  juu ya masuala mbali mbali ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii na haswa majukumu ya Mamlaka .Semina hiyo   ya siku mbili imehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka katika mifuko yote ya hifadhi ya Jamii Tanzania Bara , Wawakilishi kutoka  wa Shirika la Nyumba ya Taifa  ( NHC ), Wafanyakazi wa  Bodi ya Mishahara  na  wawakilishi kutoka mfuko wa  Bima ya Afya
 Mkurugenzi wa  Ufuatiliaji na uandikishaji  Bi. Lightness Mauki akiwasilisha  mada kuhusiana na Shughuli na majukumu ya SSRA
 Mdau kutoka NSSF Mr. C. Magori  akiuliza swali  na kutoa ushauri  kuhusiana na  majukumu ya Bodi ya Mikopo
 Katibu Mtendaji  Wa Bodi ya Mishahara  na Maslahi Katika Utumishi wa Umma  Bi. Tamika Mwakahesya akiwasilisha mada kuhusiana na majukumu mbalimbali ya Bodi ya Mishahara
Mdau kutoka NHIF  akielezea  majukumu ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...