Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unafuraha kuwataarifu abiria wote na wananchi kwa jumla kuwa, safari za treni ya abiria ya kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza zitaanza tena kuanzia Desemba 07, 2012 kwa siku za Jumanne na Ijumaa muda wa kuondoka katika Stesheni ya Dar utakuwa saa 8:30 mchana badala ya saa 11:00 jioni. 

Hivyo basi , Mwananchi yeyote anayetaka kusafiri kwenda Mwanza anaweza kununua tiketi yake wakati wowote katika Stesheni iliyo karibu naye. Tafadhali atakayesoma taarifa hii amuarifu na mwenzake!

. Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya
Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Kipallo Aman Kisamfu
Dar es Salaam
Novemba 29, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. mbona suala na madaraja ya tiketi hawasemi?! Awali treni toka Dar ilikuwa na 3rd class tu. Je na 2nd itakuwepo.

    Safari za treni zinanikumbusha miaka ya 80 nilipokuwa sekondari nikitumia warrant. Usafiri salama kuliko basi tatizo waweza kutumia siku 5 kwa safari ya masaa 24!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...