Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unawatangazia abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa, safari za treni ya abiria ya kutoka Dar es Salaam kwenda Bara kuanzia Desemba 4, 2012 zitakuwa zikiondoka saa 8:30 mchana kila ya siku ya Jumanne na Ijumaa. badala ya saa 11:00 jioni hii inatokana na sababu za kiutawala ikiwemo kutoa nafasi ya uratibu wa huduma mpya ya treni ya jiji la Dar es Salaam ilioanza Oktoba 29, 2012. Hata hivyo kwa treni kutoka Kigoma na Mpanda muda wa kuondoka Katika  stesheni hizo utabaki kama ulivyo katika ratiba ya sasa. 
 Tafadhali atakayesoma taarifa hii amuarifu na mwenzake.
Uongozi wa TRL unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya
Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Kipallo Aman Kisamfu
Dar es Salaam
Novemba 24, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...