Rais mstaafu wa Afrika ya Kusini, Mh. Thabo Mbeki (pichani) anatarajiwa kuhudhuria mkutano utakaojadili maswala ya uongozi Afrika jijini Dar es Salaam kesho asubuhi.
Mkutano huo uliotayarishwa na UONGOZI Institute kwa kushirikiana na Thabo Mbeki Foundation unahusisha wadau mbalimbali muhimu watakaojadiliana kwa uwazi kuhusu wajibu wa uongozi na mustakabali wa bara la Afrika.
“Hatuna nia ya kujenga dhana ya uongozi kwa bara la Afrika, lakini majadiliano ya uwazi ya uongozi unaotakiwa kushughulikia changamoto za maendeleo katika bara hili ni muhimu,” alisema Afisa Mtendaji Mkuu wa UONGOZI Institute, Prof. Joseph Semboja jana katika taarifa.
Kwa mujibu wa taasisi hiyo, mazungumzo hayo yanalenga kwenda mbali zaidi ya kuangalia changamoto zinazoikabili Afrika pamoja na kukosoa uongozi lakini hasa kuangalia maswala yanayohusu aina ya viongozi wanaotakiwa pamoja na matayarisho yanayohitajika ili kupata viongozi hao wenye uwezo na mbinu za kuwawezesha kuongoza.
“Ni muhimu kwa Afrika kuwa na viongozi wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za leo na kuwezesha bara hili kusonga mbele,” alisema Prof. Masanja.
Mazungumzo hayo pia yatajadili uwezo wa viongozi kutekeleza maswala mbalimbali kwa nyenzo na raslimali walizonazo, hali ya taasisi na kama mazingira ya ndani na nje ya bara la Afrika yanasaidia au kuzuia viongozi katika bara hilo kufanikisha malengo yao.
UONGOZI Institute hutayarisha mikutano kama hiyo na kuwakutanisha viongozi kwa lengo la kujadili mada mbalimbali ili kufikia malengo ya maendeleo endelevu Afrika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Rais Mstaafu Mbeki tuna wezaje kusikia mkutano huu kuhusu uongozi kwenye bara la Afrika?Mara kwa mara tuna soma habari za mikutano lakini hakuna details.Je mkutano huu uta patikana kwenye youtube, Asante.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...