Nilitoa  tangazo  kuwa kijana mmoja wa  kisomali  anautafuta ukoo  wake na  nilifanikiwa  kukutana na   mhusika  mmoja  ambapo  alikuja   nyumbani  na  kumweleza   kila  kitu  pamoja  na   mahali  alipo  huyo  kijana na  aliaidi kumpelekea  ujumbe  huo  muhusika  mkuu anayeitwa  HUSEIN  ALLLY  mkazi  wa  makuyuni ,arusha ambaye  ndiye  baba wa huyo  kijana.

Cha  ajabu  ni  kwamba  mpaka  sasa mzazi  huyo  hajatokea wala  kufanya  mawasiliano  yoyote  na  sisi  mana tulimweleza  kuwa  asiwe  na  wasiwasi  na sisi  ili  akamchukue  mtoto wake   kwani anaishi  katika   mazingira  magumu  mno .

Nawaomba  ndugu  zangu  wasomali  msiwe  na  roho  za  kikatili  kwa  kuwatenga  watoto  wenu  mliozaa nje  ya  ndoa kwa  wanawake  wasio wasomali. Namuimiza  sana  huyo  mzee HUSEIN ALLY akamchukue  mtoto  wake  tulipomwelekeza  alipo  mana damu  ni  nzito  kiliko  maji.

Mdau Makuyuni, Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. mdau kazi umeipitisha na wajibu wako umeufanya mwenyezi mungu atakulipa kila la kheri

    twengepata watu kama nyinyi mwenye moyo na imani hii mzuri basi hii dunia ingekuwa ndio pepo

    ila usijali mungu atakulipa na utaongezewa barka kwenye mihangaiko yako ndugu yangu kuanzia kesho ishallah utakuta mambo yako yanazidi kuwa mazuri kwa wema wako nakutakia usiku mwema

    ReplyDelete
  2. Unataka kuniambia watanzania hawana tabia hiyo? Acha ubaguzi, ongelea tabia, sio kabila! hao watoto wanaotupwa majalalani kila kukicha ni wakisomali?

    ReplyDelete
  3. Katika Imani ya kiislamu huyo si mtoto wake,(mtoto wa nje ya ndoa ni mtoto wa mama) hivyo hapaswi kulazimishwa kwenda kumchukua, tena kwenye vyombo vya habari kama hivi. Pili ume-generalize kwamba eti wasomali waache roho za ukatili za kutupa watoto, sio kweli wasomali hawana tabia hiyo bali hiyo ni Tabia ya mtu.Hata wewe unaweza ukawa nayo.
    Kama ujumbe atakuwa kaupata basi vuta subira anaweza kufanya hisani ya kuja kumchukua huyo mtoto na kumlea na sio kumlazimisha kumchukua. Hili ni jambo la ghafla na pengine anahitaji kujipanga kabla ya kufanya hiyo hisani.

    Ni hayo tu.

    Mdau Kisiju Pwani.

    ReplyDelete
  4. kwa akili yako ukibandika post na kashfa ndo atafanya?

    jifunze kuwa na lugha nzuri inayofanya malengo yako yatimie.

    mpaka umejuwa kutembelea blog lakini hujajua kauli njema.

    ReplyDelete
  5. Kwa kweli Huna busara kabisa utawachanganya Vp wasomali Wote Kwa swala hili unataka kuniambia hao watoto wanao omba omba Kila kona ya hiyo nchi Ni wasomali? Think before you talk, do a DNA test ndio uongee unasema kama Huna kichwa. Watu kama wewe ndio wanao anzishaga vurugu ktk nchi.

    ReplyDelete
  6. from the negative posts above utajua tuu hao wote ni wasomali.

    Kwa hiyo tumsifie kwa kumtupa mwanae?!! au tumseme na kukemea hii tabia?

    bahati mbaya, tabia za wasomali wengi zinajulikana! huhitaji darubini wala DNA kujua.

    Shida sana... sijui tutafika lini?

    ReplyDelete
  7. Huyo alosema mtoto aw nje ya ndoa ni mtoto wa mama since when?usisingizie Imani tumia akili yako maana hiyo Imani pia inakataza zinaa nae kazini na mwanamke asiyefunga nae ndoa,maji yashamwagika,mtoto kashazaliwa Hana hata kosa,huyo jamaa achukue kiumbe wake kuliko mtoto aendelee kumangamanga mtaani,na mtoa taarifa kasisitizia swala la usomali kwasababu kidesturi wasomali hawaoani na waswahili ni nadra siyo common kuona couple za kisomali +kiswahili naamini Hana nia mbaya.Hata hivyo Kama tungejitahidi kuchukua watoto tunaowazaa nje ya ndoa na kuwapa elimu bora na malezi bora naamini watoto hao wangekuwa na maisha mazuri na ya furaha,kwanini tuache watoto wetu wakitaabika bila elimu,upendo,malezi bora ilhali ni wetu hata Kama tumewazaa nje ya ndoa,tuwachukue Hawana hatia hao,kosa ni letu sie wazazi

    ReplyDelete
  8. Mtu kama huna point yeyote ya maana ya kuzungumzia ni bora uweke maoni yako na hisia zako mbali na mjadala. Huwezi kuropoka tuu mradi umezungumza. Sasa huyu bwana anaedai hao wote waliopinga kauli ya kujumuisha wasomali wote ni wasomali and they are negative. Unaposema tabia za wasomali wengi zinajulikana!. Huoni kwamba unajumuisha jamii nzima na wewe mwenyewe una-sound so negatively. Na pia unakuwa umetoka njee ya mada kwa kuingiza hisia zako kwa kudai eti unazijua tabia za wasomali wengi kwani jamii nzima walikutia mimba wewe na kukuacha msele mpaka ukazijua tabia zao?.Hapa unatakiwa uchangie jinsi ya kumsaidia au kuwwawezesha huyo kijana na huyu mzazi alieshindwa kutimiza wajibu wake kuwa pamoja au jinsi ya kumsaidia huyo mtoto. Sio uendeleze misjudgements and negativity by painting the whole community badly. Watu kama wewe na huyu mdau wa Makuyuni wenye upeo finyu wa kimawazo kwa kudai kosa la mtu au watu wachache basi unahukumu jamii nzima ndivyo ilivyo. Mnakosea na mnatakiwa mfikirie kabla hujasema au hujaandika.
    By the way mii sio msomali!

    ReplyDelete
  9. Baba wa mtoto Hussein Ally alikuwa na azma njema ya kuoanana na mwanae alipopewa taarifa isipokuwa alipangwa kujiunga na Wapiganaji wa AL SHABAAB na sasa yupo Somalia huku wakiwa wamezingirwa na Majeshi ya Serikali ya Somalia (Somali National Ermy-SNA) !

    Sasa wandugu atachomoka vipi huko Somalia ili kurudi hapo Mombo/Makuyuni-Tanzania kwa mwanaye?

    ReplyDelete
  10. I know have seen this post 4 years letter , Mi msomali mkenya na utu hauna kabila.

    Ali Hussein a-take responsibility!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...