Mhe. Mathias Chikawe (MB) Waziri wa Katiba na Sheria leo tarehe 18/12/2012 amefungua Warsha ya Viongozi wa Dini kuhusu nafasi ya Dini katika kulinda na kudumisha amani Nchini.
Warsha hiyo iliandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari, Uhalifu wa Kivita, Uhalifu dhidi ya Binadamu na aina zote za Ubaguzi ambayo iko chini wa Wizara ya Katiba na Sheria.
Warsha hiyo ina lengo la kuyajengea uwezo makundi mbalimbali katika jamii na kuleta uelewa wa ujumla wa wananchi kuhusu vyanzo, madhara na namna ya kuzuia mauaji ya kimbari, hii ni pamoja na kupinga vitendo vyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani ikiwa ni pamoja na ubaguzi, matamshi ya kichochezi na kunyamazia mambo kwa vyombo husika.
Mhe Chikawe aliwataka viongozi wa Dini zote kuendelea kukemea vitendo vya kibaguzi, vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani.
Pia kutumia warsha hiyo kubaini na kujadili kwa amani vyanzo vya chokochoko za kidini zilizoanza kujitokeza hivi karibuni na kutafuta majibu ya njia za kuzuia.
![]() |
Baadhi ya washiriki |
![]() |
Mhe. Mathias Chikawe (MB) Waziri wa Katiba na Sheria (wa pili kuumeni) leo tarehe 18/12/2012 akifungua Warsha ya Viongozi wa Dini kuhusu nafasi ya Dini katika kulinda na kudumisha amani Nchini. |
Baadhi ya viongozi wa Dini
katika Picha na Mhe. Chikawe
Ni vizuri kwa Chikawe angejaribu kuwasisitiza viongozi wenye waumini wengi. Sijawaona viongozi wa kikatoriki, lutherani, anglikana amabao uwepo wao ungeleta changamoto. Kazi njema Chikawe
ReplyDeleteMihadhara ya dini iangaliwe sana huko ndiko kunazuka chokochoko kwa nini usihubiri kwa kutumia kitabu cha imani yako na kuwafundisha waumini wako mafundisho ya imani yako?
ReplyDeleteWapige marufuku Mkristu kutumia Kurani wakati wa mhadhara na pia Muislamu marufuku kutumia Biblia kwenye mhadhara. Muda wa mihadhara ueleweke na ufuatwe, wengine huanza saa 8 mchana hadi saa 12 jioni na wengine huanza saa 12 jioni hadi saa 4 au 6 usiku kwa nini na usawa uko wapi????Tahadhari