Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Monduli juu,Mkoani Arusha wakati alipokuwa akiwasili kijijini hapo kwa ajili ya shughuli ya uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo katika kijiji cha Mfereji Monduli juu.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akifunua kitambaa kwenye jiwe la msingi kuashiria uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo,lililoko katika Kijiji cha Mfereji,Monduli Juu.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Mfereji,Monduli Juu,mara baada ya kuzindua josho la kisasa la Mifugo.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo,lililoko katika Kijiji cha Mfereji,Monduli Juu.
Mifugo ikiingizwa kwenye Josho hilo,mara baada ya kuzinduliwa.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Monduli juu,Mkoani Arusha wakati wa hafla ya uzinduzi wa josho la kisasa katika kijiji cha Mfereji Monduli juu. ambapo ametoa wito kwa wakulima na wafugaji nchini kuacha uhasama wa kugombea ardhi.

Amesema kuwa kila mtu ana haki yake hivyo ni muhimu kwa jamii hizo kuheshimiana na kukaa pamoja kutatua tatizo la ardhi kwa ajili ya malisho ya mifugo pamoja na kilimo.Kumekuwa na matokeo mengi sehemu mbalimbali ya kupigana kuwania ardhi kati ya wakulima na wafugaji, miongoni mwa maeneo hayo ikiwa ni mkoani arusha.

Amewaambia watu wa jamii ya kimasai ambao ni wafugaji kuingia katika ufugaji wa kisasa utakaowazuia kuhama hama kutafuta malisho ya mifugo yao.''Jamani watanzania wenzetu hawatakubali mtakapovamia maeneo yao bila ya ruhusa ni lazima tuondokane na tabia hii'' alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...