Rais wa Rotary Club Mzizima, Ambrose Nshala (kulia) na mwanachama mwingine wa klabu hiyo, Ailinda Sawe wakigawa keki kwa watoto wanaolelewa katika Kijiji cha SOS, wakati wanachama wa klabu hiyo walipowatembelea kuwagawia zawadi za vyakula na mafuta kwa ajili ya Sikuu za X-Mass na Mwaka mpya Jijini Dar es Salaam juzi.
Rais wa Rotary Club Mzizima, Ambrose Nshala (wa pili kushoto) akimkabidhi Lupilo Mwakajumba ambaye ni mlezi wa wa Mlezi wa watoto wa Kijiji cha SOS, sehemu ya msaada wa vyakula vilivyotolewa na wanachama wa klabu hiyo kwa ajili ya sikukuu za X-Mass na mwaka mpya, Dar es Salaam juzi.
Rais wa Rotary Club Mzizima, Ambrose Nshala (wa pili kushoto), akiwa na wanachama wengine wa klabu hiyo, Cyril Pesha (kushoto), Dedera Merinyo, Dunstan Kaijage, Dennis Mazige na Ailinda Sawe wakiwa na vyakula ambavyo walienda kuvigawa kwa ajili ya watoto wa Kijiji hicho.
Wanachama wa klabu hiyo wakitembelea nyumba zilizopo katika kijiji cha SOS, Dar es Salaam.
Wanachama wa Rotary Club, Mzizima wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wa kijiji cha SOS mara baada ya kuwakabidhi msaada wa vyakula kwa ajili ya sikukuu za X-Mas na Mwaka Mpya, hafla iliyofanyika kijijini hapo juzi.
Mwenye kujua naomba anipe sifa na maelelezo ya kujiunga na Rotary club
ReplyDelete