Kutokana na mgomo wa
madaktari uliotokea kati ya tarehe 23 na 29 mwezi juni 2012.Wizara iliwasilisha
malalamiko kwenye Baraza la madaktari Tanganyika ili lifanye uchunguzi kuhusu
madaktari hao .
Idadi ya madaktari wote waliogoma walikuwa 394, kati yao madaktari 376
walikuwa ni madaktari walio katika mafunzo kwa vitendo (Interns) kutoka hospitali
za Muhimbili, K.C.M.C. Bugando, Mbeya Rufaa, St.Francis - Ifakara, Dodoma,
Temeke, Mwananyamala, Amana, Haydom na Sekou Toure. Aidha, Madaktari waajiriwa(Registrar)
18 walishiriki katika mgomo huo
kutoka hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
Baraza
lilipitia malalamiko yote na limetoa adhabu stahiki kwa kila daktari
aliyethibitishwa kushiriki katika mgomo huo.
Adhabu hizo zilikuwa katika makundi yafuatayo; onyo, onyo kali na kusimamishwa
udaktari kwa muda wa kati ya mwezi mmoja na miezi sita.Vile vile kuna Madaktari
ambao hawakuwa na hatia ya kushiriki katika mgomo na hivyo walifutiwa mashtaka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...