Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akitoa hotuba ya ufunguzi wa jengo la ghorofa kwa ajili ya makazi ya Askari Magereza mjini Iringa. Ufunguzi huo uliambatana na sherehe kubwa ambayo iliudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na maofisa wa Jeshi la Magereza. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini CGP  John Minja

 Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akiukata utepe akiashiria ufunguzi wa jengo la ghorofa kwa ajili ya makazi ya Askari Magereza mjini Iringa.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (aliye vaa kiraia kushoto) akifunua kitambaa kuashiria ufunguzi wa jengo la ghorofa kwa ajili ya makazi ya Askari Magereza mjini Iringa. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa  Jeshi la Magereza nchini CGP John Minja.
 Baadhi ya sehemu ya nje na ndani ya jengo hilo pamoja na maafisa mbalimbali wa jeshi hilo wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya jengo hilo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akipata maelezo wakati alipotembelea vyumba vya jengo hilo
 Kamishna Jenerali wa  Jeshi la Magereza nchini CGP John Minja katika picha ya pamoja na maafisa waandamizi wa jeshi hilo baada ya ufunguzi wa jengo. PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Haya magorofa yatakua machafuuu, meusiii, fii kokodo kama yale ya mwenge pale dar es salaam kwa jinsi niwajuavyo askari wetu.
    Mtu anashindwa kupiga rangi hata balcon ambayo anaishi yeye mwenyewe kwa kusubiri jeshi au serikali ije ipige rangi.
    Taabu kwelikweli.

    ReplyDelete
  2. Asante kwa kuwakumbuka askari hawa ambao nyumba zao nyingi ni mbaya kuliko gerezani. Zoezi hili liendelee mikoa yote. Bravo!!

    ReplyDelete
  3. Uongozi wa Magereza hauna gender balance? I trust Bw Minja kwa uelewa wake baada ya UN ataliona hili na kulirekebisha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...