Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Nimesikitishwa sana na habari ya huyo mtoto. Jamani wazazi tuwe tunawaangalia watoto wakiwa wanacheza kwa usalama wao. Yaani hadi mwili umenisisimka.
    Hivi mawazo ya ushirikiana yatatuisha lini jamani? Haya sasa mna kesi ya kujibu mmeacha familia zinateseka kwa kukosa nguvu kazi kisa mawazo ya kijinga. Poleni wafiwa, Mungu awatie nguvu kwa wakati huu mgumu.

    ReplyDelete
  2. Inasikitisha sana kuona bado sehemu kubwa ya watanzania wanaamini nguvu za giza.Huko nyumbani watu wengi wanaamini kuwa vitu kama mvua, jua, mafuriko, upepo, radi au hata vumbi vyaweza kutengenezwa na binadamu ktk mazingira ya uchawi.Kuna makala moja nilishawahi kuisoma kuwa radi za kutengenezwa zinauzwa kule shinyanga.Nadhani kuna haja ya kuliangalia hili kwa macho yote mara nyingi wahusika wanatumia mwanya wa serikali kujinasibu kwamba haiamini ushirikina kuendeleza hofu miongoni mwa wananchi wenzao.Mbaya zaidi huwa nasoma hata kwa watoto ambao huzaliwa wakiwa na kasoro za maumbile watu huwa wanapigana mapanga na hata kuchomeana nyumba zao.Kuna haja ya kuhamasisha uelewa wa wananchi juu ya elimu ya asili na uwezekano wa kutokea yote haya kwa kuwapa uthibitisho wa kitaalamu kwani wamekosa nafasi ya kuelimika.

    ReplyDelete
  3. Imani za Kishirikina zitatuweka Tanzania kuwa Karne ya 12 wakati tumeshaingia ktk karne ya 21!

    Nimeshuhudia Mkazi mmoja wa Gongo la mboto Jijini Dar akilalamika ya kuwa alifanyiwa fujo na Majirani zake waliopanga wote nyumba moja kwa madai ya kuwa jamaa ni Mchawi kwa kuwa haishiwi na hakopi, wahkadai jamaa ana Hela za Majini anayofuga, ikabidi jamaa ahame baada ya mzozo huo.

    Mtu mwingine Mkazi wa Mbagala alisema Wapangaji wenzake wanamwita 'Chuma ulete' kwa kuwa Jamaa pia analipa Kodi kwa Mwaka badala ya miezi na kuwa yeye ndiye anawasababishia ugumu wa maisha wenzake hapo ndani, wanauliza wakiwa hawana yeye mwenzao anapata wapi fedha?

    Wengine walidiriki kuhama, lakini jamaa bado yupo anaomba Mungu wasije amu siku kumvamia!

    Hivi wandugu, hamkumbuki Mhe. Raisi Kikwete muda mmoja zilivyo vuma imani za Kishirikina aliwahi kuwahutubia wakazi wa Kanda ya Ziwa ya kuwa Utajiri unakuja kwa kuchapa kazi na kuwa na Uadilifu kwenye maamuzi na matumizi ya fedha?, badala ya kuua Vikongwe na Maalbino ili kuongeza uwezo wa Kifedha na Kupata Utajiri !!!

    ReplyDelete
  4. Ohhh nafikiri wakazi wa Kijiji hiki kama suala ni mvua wangemfuata Mhe. Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.

    Mhe.Lowassa alisimamia Mpango wa kuleta mvua za Kitekinolojia kutoka nchini Thailand na kwa vile Mhe.Lowassa anatokea kwenye Jamaa ya kimasai amabayo hufuga na kushirikiana na wakulima hatosita kuwapa ushirikiano badala aya kuuana wenyewe kwa wenyewe kutokana na tuhuma za uchawi eti kisa?...mvua !

    ReplyDelete
  5. Wakazi wa Kijiji amkeni hii ni Karne ya 21 muwe Kisayansi zaidi kuliko Kiushirikina!

    Ohhh, ninyi 13 mlioshikiliwa na huyo mmoja aliyetoroka Mutafungwa!

    ReplyDelete
  6. No,jamani,vijijini bado saaaanaaaa,wala tusipuuzie!hali ya maisha ni mbaya!Patahitajika nguvu ya pamoja,taasisi zote kwa pamoja,za Kidini,za Serikali na zisizo za serikali,kwa pamoja,kulikabili tatizo hili.Kiini chake ni Ujinga na pacha wake Umaskini!ndiyo wanaozaa Maradhi na Kupoteza Matumaini ya Uhai!tuamke na kuchukua hatua sasa,badala ya kuendelea kunyoosheana vidole!na baya zaidi,gonjwa hili sasa limewaingia vijana,na sio vikongwe!tunakwenda wapi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...