Mgeni mmoja raia wa Ireland anayefahamika kama Ian Mc Keever amefariki dunia jana tarehe 2.1.2013 majira ya saa sita na nusu mchana  baada ya kutokea kwa ajali ya radi kali wakati akipanda Mlima Kilimanjaro akiwa pamoja na wenzake.

Ajali hiyo ya radi ilitokea katika eneo la Kibao cha Moir Hut katika njia ya Londorosi. Aidha, wageni wengine wanne walijeruhiwa katika ajali hiyo.

Marehemu Mc Keever mwenye umri wa miaka 42 alifika nchini kwa ajili ya shughuli ya utalii ya kupanda Mlima Kilimanjaro kupitia Kampuni ya Wakala wa Utalii ya Everlasting Tour Company Limited ya Mjini Arusha ambapo marehemu pamoja na wenzake walianza safari yao ya kupanda mlima tarehe 30.12.2012

Baada ya kutokea kwa ajali hiyo wageni wengine 21 waliokuwa pamoja waliamua kuahirisha safari yao ya kupanda mlima.

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Wakala wa Utalii ya Everlasting zinaendelea na taratibu mbalimbali za kushughulikia ajali hii pamoja na matibabu kwa waliojeruhiwa.

Imetolewa na

Pascal Shelutete
Meneja Uhusiano
HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Ni mapenzi ya Mungu

    David V

    ReplyDelete
  2. ajali ya radi inashughulikiwaje jamani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...