Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan (kulia), akimkabidhi funguo mshindi wa Toyota Noah, Ramadhan Salum Pazi.
Idd Azzan (kulia) akimkabidhi faili la gari mshindi wa Noah, Ramadhan Pazi.
Ramadhan Pazi akiingia katika gari lake aina ya Toyota Noah.
...Akiwa ndani ya gari lake.
Idd Azzan akimsaidia Pazi kuwasha gari lake.
--
MSHINDI wa Bahati Nasibu ya 'Timiza Ndoto Yako, Jishindie Toyota Noah' ambayo ilikuwa inaendeshwa na Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd, Ramadhan Salum Pazi, mkazi wa Buguruni-Rozana jijini Dar es Salaam, leo amekabidhiwa gari lake aina ya Toyota Noah.

 Makabidhiano hayo yamefanywa na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan nje ya ofisi za Global Publishers. 

Bahati Nasibu hiyo iliyokuwa inaendeshwa kupitia magazeti ya Global ambayo ni Uwazi, Risasi, Championi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda ilifika mwisho Desemba 20 mwaka jana ambapo bwana Ramadhani Pazi aliibuka kidedea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. HIYO BAHATI NASIBU YA KWELI AU YA KUPANGA MATOKEO MBONA ALIYESHINDA HANA FURAHA KABISA WALA SURA YAKE HAIONYESHI KUSHINDA KAMA VILE ANALAZIMISHWA KUSEMA YEYE NDIO MSHINDI MAANA BAHATI NASIBU ZA MJINI WASHINDI HUWA WANAJULIKAMA MAPEMA HUENDA YEYE NI RUBBER STAMP TU HAPO BINAFSI NINA WASIWASI NA USHINDI WAKE TUTAMUONA NALO MJINI KAMA KWELI KASHINDA!!

    ReplyDelete
  2. mtu unapata zawadi unashindwa hata kuonyesha jino moja, umenunaaaaaaaaa au mshindi wewe ulikuwa unataka vogue sport? ha ha haaaa.. wenzako wanashindi bajaji unaona meno yote hamsini mdomoni.

    ReplyDelete
  3. Opossum (Didelphis Virginiana)aka The North America Opossu, wa MEXICO wanamuita Tlacuache, ndiye mnyama pekee mwenye meno HAMSINI, sisi binadamu tuna meno 32 tu, kama hujan`goa hata moja, au hujapoteza meno kilabuni!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...