Habari iliyotufikia hivi punde inaeleza kuwa kundi
kubwa la wananchi waliojawa na ghazabu Wilayani Rufiji leo wamevamia
kituo cha Polisi Kibiti Wilayani humo na kuanzisha vurugu kubwa kufuatia
raia mmoja mkazi wa kijiji hicho kudaiwa kufa kwa kile kilichodaiwa
kuwa ni kutokana na kipigo cha Polisi.
Chanzo
chetu cha Habari kutoka Kibiti kinatupasha kuwa,kijana huyo aliyefariki
kutokana na kipigo hicho afahamikae kwa jina la Hamis Mpondi ambaye
mauti yamemfika wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili,jijini Dar es Salaam na taarifa hiyo ilipowafikia wananchi hao
ndipo wakachukua uamuzi wa kwenda kituoni hapo na kuanzisha vurugu
hizo.
Habari
zaidi zinaeleza kuwa,hivi sasa wananchi hao wanateketeza nyumba za
Askari Polisi hao zilizopo jirani kabisa na kituo hicho, licha ya juhudi
za Polisi kuwatawanya kwa mabomu kuendelea kufanyika.
Aidha
wananchi hao wameanza kufunga barabara kuu ya Kilwa iendayo Mikoa ya
Kusini, Lindi na Mtwara kwa mawe, magogo na kuchoma matairi ikiwa ni
umbali wa kama kilometa moja kutoka kituo cha Polisi Kibiti.
Inaelezwa
kuwa hali imezidi kuwa tete katika eneo hilo huku Polisi wa Kibiti
wakiendelea na jitihada za kudhibiti hali hiyo kwa kufyatua mabomu ya
machozi hewani kujaribu kutawanya umati huo wa watu.
tutaendelea kupeana taarifa zaidi kadri zitakavyokuwa zikitufikia.
Polisi wetu hawajui wajibu wao.
ReplyDeleteImefika wakati warudishwe shule ili angalao waelimike.
Yaani hawajui wanadfanya nini.a
Jamani askari chonde chonde musionee raia sasa watu wamejawa na hasira na matokeo yake itakuwa ni hasara.
ReplyDeleteJeshi la polisi tunawaomba mufikirie hao munaowaajiri siyo wakipewa silaha ndiyo waone wanaweza kuzifyatua tu au kupiga watu mpaka kufa.
Wananchi wamechoka na uonevu wa askari sasa.
haiingii akilini mtuhumiwa anapelekwa polisi akiwa mzima halafu mauti inamkuta akiwa kituoni kwa ku[igwa na maafande, huku wananchi tunaambiwa tusichukue sheria mkononi kuuwa vibaka huko polisi nako wanachukua sheria mkononi na kuuwa, nini maana ya mahakama? ikiwa jeshi la polisi linaua mtuhumiwa naona hakuna haja ya mahakama. ninawaunga mkono, miguu na kichwa wananchi walioteketeza nyumba zenu, yani nyinyi polisi wa bongo inabidi wote muende israel mkajifunze upolisi. zaidi mnachojua ni rushwa na mabavu, kuua raia kwa makusudi, ubabe mwingiiii kichwani 0, mkishavaa hayo magwanda yenu mnajiona miungu watu. na sio rufiji tuu hii tabia ya kuua raia vituoni ipo tanzania nzima, hii kitu lazima iingizwe kwenye katiba mpya, kuwa polisi akiuwa raia kwa kipigo adhabu yake ni KUNYONGWA!!!
ReplyDeleteHii nimeipenda saaana na ndio inavyotakiwa hasa ili jeshi na polisi wa tanzania wapate funzo sio kuonea watu kila siku kwa kutumia nguo zao
ReplyDeleteati askari ila kama tukiendelea kupeana kipigo na tukakirudisha kwao kisawa sawa hasa basi lazima heshima itakuwepo na hapa kimaoni yangu haina haja ya kuharibu jengo wameuwa mtu mmoja na sisi tuuwe askari mmoja tu
sio zaidi ili tuwe sambamba nao tusiwadhulumu wala wasitudhulumu HAKI SAWA KWANANI .....SOTE
hii ni hali mbaya sana, imani ya wananchi kwa polisi imekwisha kwa kuwa matendo ya polisi kupiga na kuua raia yanaongezeka bila kuchukuliwa hatua kali kwa hiyo wameamua kuchukua hatua wenyewe!!!Nchi ikifikia hapo ni balaa tupu hasa kwa kuwa polisi wengi wanaishi uraiani.
ReplyDeleteMaumivu ya kichwa huanza polepole.......
ReplyDeleteSasa kama ingekuwa gesi ipo Kigoma au Petrol iko Ruvuma nyinyi watu wa Mtwara na Lindi msingetaka kodi iwanufaishi Watanzania wote? Raia wa TZ anahaki ya kuishi popote. Kama anaona sehemu fulani ya TZ angehamia ili aishi vizuri basi afanye hivyo. Viwanda vitajengwa pale ambapo kutalate faida zaidi kwa kuangalia ammbo mengi.
ReplyDeleteBado yatatokea mengi! Watu wana hasira siku hizi!
ReplyDelete