Siku kadhaa zilizopita timejionea wenyewe tena kwa macho yetu Mamlaka ya Mawasiliano Nchini Tanzania (TCRA) ikiamua kuingia
rasmi katika Mfumo wa kurusha Mawasiliano ya Televisheni na Redio katika mfumo wa kisasa wa Dijitali kutoka ule mfumo wa zamani wa Analojia, kwa upande mwingine leo Shirika
la Usambazaji Umeme TANESCO nao wameamua kuingia katika Mfumo huo wa
Dijitali kwa staili yao ya kipekee kwa kupandanisha nguzo ya Umeme katika mti halisi
ambao bado unamea kama jinsi taswira hizi zinavyoonesha. Taswira hii imepatikana Huko Mkoani Ruvuma, na TANESCO mkoani humo wameamua kutumia njia hii kurahisisha usambazaji umeme.
Jionee jinsi Tanesco walivyo na teknolojia ya kisasa katika kipindi hiki cha Mwaka 2013.
Jiulize kwa hali kama hii Tanesco wako juu kwa mfumo huu au wanajaribu nao mfumo wao mpya?.Picha na Demashonews Blog
Kuna siku nilimuuliza rafiki yangu (mhandisi-tanesco)huwa wananchi wanakupokeaje ukijitambulisha kama mhandisi wa umeme na unafanya kazi tanesco? Alinijibu kuwa wananchi wanaelewa kosa si la wafanyakazi, tena eti huwa wanampa moyo na kuwapongeza kwa jitihada zao binafsi za kuhakikisha huo umeme kidogo wanaupata japo kwa mgao. Kweli nimeamini, ni jitihada binafsi.
ReplyDeletetanesco watawamaliza kwa kuwauwa hiyo style ni mbovu sana kuna siku kutakuja kutokea milipuko mikubwa na kusababisha hatari kubwa sana serikali wacheni kucheza na raia wema.
ReplyDeleteNguzo hizi zipo Mbuji Mpya na sio Tz. kama Michu anavyodai!
ReplyDeleteJamani kama hatuwawezeshi kwa kulipia huduma wanazotoa na kubaki kufanya hujuma lukuki ikiwemo wizi wa umeme mnataka wafanye nini? Kwanza wanastahili pongezi kwa kuwa wabunifu kiasi hicho kuliko kuona wananchi wanakosa huduma.
ReplyDelete