Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Jospeh Warioba (kulia) akiongea na Mawaziri leo katika ukumbi wa ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es Salaam katika mkutano uliolenga kupata maoni ya Mawaziri kuhusu Katiba Mpya.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Nyamrunda akiongea katika mkutano kati ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Makatibu Wakuu uliolenga kupata maoni yao kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali wakifuatilia mkutano kati yao na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliolenga kupata maoni ya Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiongea katika mkutano kati ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Makatibu Wakuu uliolenga kupata maoni yaokuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Mawaziri Steven Wassira, Kapteni (Mstaafu) George Mkuchika na Prof. Sospeter Muhongo wakifuatilia mkutano kati yao na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliolenga kupata maoni ya Mawaziri kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angellah Kairuki akiongea katika mkutano kati ya Mawaziri, Manaibu Mawaziri na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliolenga kupata maoni ya Mawaziri kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali (Mstaafu) Joseph Simbakalia akiongea katika mkutano uliofanyika katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo kati ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Wawakilishi wa Wakuu wa Mikoa uliolenga kupata maoni yao kuhusu Katiba Mpya. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abass Kandoro, Dkt. Rehema Nchimbi (Dodoma) na Bi. Chiku Galawa (Tanga).
Wawakilishi wa Wakuu wa Mikoa nchini wakipata maelezo kuhusu mfumo wa uhifadhi wa maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya yanayowasilshwa katika Tume kwa maandishi kutoka kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume Bi. Flora Mkonya leo (Jumanne, Jan 15, 2013) katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia Kanali (Mstaafu) Joseph Simbakalia(Mtwara), Bw. Abass Kandoro (Mbeya), Bi. Chiku Galawa (Tanga).na Dkt. Rehema Nchimbi (Dodoma).Wakuu hao wa mikoa pia waliwaslisha maoni ya Wakuu wa Mikoa kuhusu Katiba Mpya.
Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bi. Al-Shymaa Kway-Geer, Bw. Humphrey Polepole na Bi. Riziki Mngwali wakifuatilia mkutano kati ya Tume na Mawaziri uliolenga kupata maoni ya Mawaziri kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...