Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa
 Gari la  Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa likiwa limebonyea kwa ubavuni baada ya kupata ajali Jumapili asubuhi.
-- 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa Mh. Edward Lowassa amenusurika kifo, baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupata ajali eneo la Bwawani mkoani Morogoro.

Gari hilo la Mhe  Lowassa liligongwa na basi la Morobest, wakati basi hilo lilipolipita basi jingine kwenye daraja na kukutana uso kwa uso na gari lakini dereva wa  Mh. Lowasa kwa ustadi mkubwa alilikwepesha gari lisigonge upande alipokuwa amekaa  mzee na kuligonga ubavuni nyuma kwa upande wa dereva na hakuna aliyejeruhiwa.


Mhe Lowassa na msafara wake aliendelea na safari hadi morogoro ambako ameshiriki katika harambee ya ujenzi wa kanisa la KKKT Kilakala ambapo yeye na Marafiki Zake Wamechangia Shilingi Milioni 18

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. Sio dreva kwa ustadi mkubwa, ni Mungu aliepusha, tujifunze kumweka Mungu mbele kabla ya kuongelea ustadi wetu.

    ReplyDelete
  2. Haihusiani na mungu wala nini! kama ingekuwa hivyo basi waumini wasingekuwa wanapata ajali... madereva wawe waangalifu tu barabarani na NDIYO, ustadi muhimu kuliko imani!

    ReplyDelete
  3. Amina mdau wa kwanza.

    ReplyDelete
  4. pole sana rais wetu mtarajiwa,alah ni mkubwa

    ReplyDelete
  5. Kwahiyo dreva alitakiwa atulie tu amwachie mungu?

    ReplyDelete
  6. duu mtaani huku kila kona lowasa yupo nairobi mahutihuti
    at list umetupa habar kamili

    ReplyDelete
  7. POLE MHESHIMIWA LOWASA.

    ReplyDelete
  8. Mdau wa kwanza umenena!

    ReplyDelete
  9. Ehhh,

    Jamani Morogoro ina mzimu gani na Mawaziri Mkuu wetu?

    Mwaka 1984 tuliomboleza, na leo yanatokea haya tena!

    Au ni kwa sababu ya Mlima Kolelo?

    ReplyDelete
  10. Naungana na mdau wa kwanza. Ni bahati mbaya kuona watu tunamsahau Mungu kwa matukio kama haya na kujichukulia stahiki isiyowastahili, siyo ustadi mkubwa wa dreva bali ni mkono wa Mungu uliowanusuru. Ni madreva wangapi wenye ustadi ukubwa ambao wamepoteza maisha yao kwenye ajali. Tujifunze na kukumbuka kumshukuru Mungu kwa kila jambo

    ReplyDelete
  11. naungana na mdau wa hapo juu 100 kwa 100

    ReplyDelete
  12. Hajakosea hata kidogo.Umahiri wa dereva ndio uliofanya wanusurike.Mungu anawezesha katika jitihada zetu.Ndio maana Mungu anasema niiteni nami nitawaitikia,bisheni nanyimtafunguliwa. Jitihada zetu ndizo Mungu anatufanyia.Kama wengine wanakufa katika ajali kwa nini Mungu huyo asiwanusuru basi? ufanye uzembe useme Mungu atakuokoa?kwa nini tunaajili wadereva walio na sifa njema katika udereva na kufuzu kozi kama kila dereva anaweza kuendesha na Mungu akamsimamia tu?

    ReplyDelete
  13. I love this discussion!. Kila kitu tumuachie Mungu, sasa akili katupa za nini?. Walioendelea wanatumia akili Mungu alizowapa(waChina, Wajapan, waZungu), sisi tumekalia Mungu atusaidie. Tutumie akili na uwezo aliotupa, tusimuachie mzigo wote mwenyewe!!

    ReplyDelete
  14. ANON WA Tue Jan 29, 09:08:00 AM

    "Walioendelea wanatumia akili mungu alizowapa"

    Wachina- Akili zao ziliwapeleka kuona uzazi ni mtoto mmoja tu, kuna msiba mkubwa uko mbele yao. Athari ya hizo akili zinapelekea uchumi wao kuporomoka baada ya muda sio mrefu. Maana kizazi kinachozalisha na kulipia kodi hakitakuwepo kwa muda Fulani. Na wenyewe wanalijua hili.

    Wajapani- Pamoja na akili zote, wanaangamizwa kila mara, kwenye misiba yote inayowakuta huwasikii kumtaja mungu hata mara moja. Tafakari.

    Wazungu- Wanafilisika na akili zao zooote, why? Dhulma!

    Afrika?- Mtu kitu kidogo tu, ama "mama yangu wee" AU "ee mungu nisaidie". Mitikisiko kwetu tunadunda tu.

    Vyovyote itakavyokuwa, Mungu lazima atangulie mbele kwanza, jitihada zetu zinafuatia. Sio kinyume chake. Mungu hana mzigo unaomshinda.


    ANON WA Mon Jan 28, 10:08:00 PM

    Madereva wangapi "mahiri" wanaumia? Siku ya kufa nyani miti yote inateleza! hakuna cha umahiri hapo, mungu mwanzo umahiri unafuatia. Kuhusu kifo, siku ikifika utaondoka tu, kama siku yako bado, na mwenyewe mungu hajataka hata uchubuke ndio yatatokea haya ya Mh. Lowassa.





    ReplyDelete
  15. Tunachosema hapa ni kumtanguliza Mungu kwa kila jambo, hii haina maana kuwa tufanye uzembe na kudai kwamba Mungu atatusaidia/tuokoa na ajali. Dreva anauhodari gani wakati pumzi yake iko mikononi mwa Mungu. Nasisitiza tena na tena Mungu kwa uhodari wetu baadae

    ReplyDelete
  16. Pole mheshimiwa na kila la kher ktk shughuli zako

    ReplyDelete

  17. Amina!
    Mungu ametupa utashi na mengine mengi. Mungu yupo nasi daima. Angetutelekeza kwa kile alichokwisha tupatia, Shetani angechukua usukani. Hivyo basi Mungu yupoa nasi. Dereva alikuwa mcha Mungu na ndiyo maana wakati wa tukio akaweza kukwepea alikokwepea na wote kupona. Ubarikiwe sana Dereva. Endelea kumuweka Mungu Mbele.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...