Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (wa pili kushoto) akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM mkoa wa Tabora waliofika kwenye Stesheni ya treni ya mkoa huo kuupokea ujumbe wa Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,unaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana sambamba na Katibu wa NEC,Itikaji na Uenezi CCM,Nape Nnauye wakiwaaga Wanachama wa CCM maeneno ya Stesheni ya Seranda,wilaya ya Manyoni mkoani Singida.wakati ujumbe wa Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,unaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM ulipopita eneo hilo mchana wa leo.
 Vijana wa Chipukizi Wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida wakimvisha skafu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana wakati alipofika kwenye Kituo cha Treni cha Saranda mkoani humo na kuzungumza na WanaCCM wa Manyoni.Mh. Kinana na Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM wako safarini kuelekea Mkoani Kigoma kwenye Maadhimisho ya Miaka 36 ya CCM.
"Bai Baii.........!! "hivi ndivyo Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana sambamba na Katibu wa NEC,Itikaji na Uenezi CCM,Nape Nnauye walivyokuwa wakiwaaga wanaCCM wa mji wa Saranda,Wilayani Manyoni.
Dkt. Asha-Rose Migiro akisalimiana na WanaCCM wa Manyoni.
Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wanaCCM wa Manyoni,Mkoani Singida wakati waliposiama katika kituo cha Saranda.
Mbunge wa Jimbo Manyoni,Mh. John Chiligati akizungumza.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi CCM,Nape Nnauye akizungumza na WanaCCM wa Manyoni leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na WanaCCM wa Manyoni leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Endeleeni na jitihada hizo viongozi wa ccm, 2015 tunataka ushindi wa kishindo na kusambaratisha upinzani wa chama fulani.

    ReplyDelete
  2. Hivi CCM hilo treni wamekodi au treni hilo linafanya safari hii kama safari nyingine? Namaanisha safari za kawaida. Naomba ufafanuzi.Picha ninayopata mpaka sasa ni kama vile mtu aliyekodi teksi.

    ReplyDelete
  3. Hivi ukiwa kwenye train hauruhusiwi kuoga?Maana ndugu zangu wakuu nawaona na nguo zile zile wala hawajabadilisha.

    ReplyDelete
  4. We ndau hapo juu mbona majungu jamani! Zungumza mambo ya kuleta maendeleo mtu akioga au asipooga inakuhusu nini? Angalia hilo treni, angalia wanayoyafanya, angalia hali ya nchi kwa sasa! Kisha tafakari, toa maoni!

    ReplyDelete
  5. Mdau wa Tatu (3) hapo juu Sun Jan 27, 03:55:00 pm 2013

    ...wanaruhusiwa kukoga kwenye Treni?

    Kama uliliona hilo kwa nini wewe usingeandaa ndoo za maji,ndara, mataulo na sabuni ili viongozi waoge wakiwa safarini?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...