Mpango wa Taifa wa damu salama kwa kushirikiana na asasi ya Evidence of action” umezindua kampeni ya kuokoa maisha ya mama na mtoto “ MAMA YE” tarehe 17/01/2013 jijini Arusha kwa kutoa elimu juu ya uchangiaji damu na kuendesha zoezi la uchangiaji damu.


Akiongea katika uzinduzi huo Meneja wa mpango wa taifa wa damu salama Dr Effesper Nkya alitoa shukrani za dhati kwa mtu mmoja mmoja na Taasisi mbalimbali ambazo zimekuwa zinashirikiana na Mpango kuhakikisha upatikanaji wa damu salama katika hosipitali zetu.

Dr Nkya katika hotuba yake alihamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kuchangia damu kwa hiari mara kwa mara ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma ya kuongezewa damu pia aliwashauri wananchi watunze usalama wa damu iliyomo mwilini mwao ili wanapochangia, iweze kusaidia wenye upungufu wa damu. Jumla ya chupa za damu 1040 zilikusanywa katika kipindi cha siku 5 ( tarehe13 mpaka 17 januari)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...