Ziara
ya kuzindua nyimbo za wasanii walioshiriki shindano la kuimba la Epiq BSS
itaendelea tarehe 1 mwezi wa tatu, ijumaa hii katika ukumbi wa Maisha Club Dar
ambapo wasanii wote walioingia kumi bora wanatarajiwa kufanya show kali siku
hiyo.
Wasanii
hao ambao wiki iliyopita walifanya show kali katika ukumbi wa Maisha Club
Dodoma, wanatarajiwa pia kufunika Maisha Club. Wasanii hao ambao wengi wamekuwa
wakisubiriwa kwa hamu na wengi tokea shindano lilipoisha mwishoni mwa mwaka
jana wamekuwa wakizungumziwa na wengi kama wanamziki watakaofanya vizuri mwaka
huu. Wasanii
watakaofanya show Dar ni Menina Atick, Nsami Nkwabi, Nshoma, Vincent, Husna
Nassor, Geofrey Levis, Wababa Mtuka, Norman Severino pamoja na mshindi wa
milioni hamsini, Walter Chillambo.
Huku
baadhi ya nyimbo zikiwa tayari zinafanya
vizuri kwenye soko la muziki kama wimbo mpya wa Walter-Siachi,
Menina-Dream Tonight, Husna-Nawamimina, Wababa-My Wife na Nsami- Muongo usiku
huo pia utakuwa na vitu vipya kibao, pamoja na uzinduzi wa nyimbo mpya za Norman,
Nshoma, Vincent na Godfery.
Akizungumzia
show hiyo,mmoja wapo wa wasanii hao, Walter anasema wapenda burudani wa Dar
wasikose kuja kumshuhudia yeye na wasanii wengine wa Epiq BSS wakifanya vitu
vyao kwani wamejipanga kwa muda mrefu.
‘Pamoja
na wimbo wangu wa Siachi pia mashabiki watapata fursa ya kuusikia wimbo wangu
utakaoufuata siku hiyo hiyo’ alisema Walter, ambaye alifanya show kali sana Dodoma. Usiku
huo pia utapambwa na burudani kali kutoka kwa wakali wengine kama Ben Paul,
Barnaba, Linah na Rich Mavoko.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...