Wanafunzi wa chuo kikuu cha udaktari (Kilimanjaro Christian Medical University College) kutoka miaka mbalimbali na kozi mbalimbali wakishirikiana na wafanyakazi wa KCMC (kilimanjaro Christian Medical Centre) kupitia kikundi chao kiitwacho Shine Light wameweza kukusanya shillingi Milioni mbili na Laki saba na kuweza kuwasaidia wanafunzi 23 kutoka kituo cha kulelea watoto wanaoshi katika mazingira magumu kwa ajili ya masomo yao,wameweza kuwanunulia sare za shule (mashati,masweta,kaptura,sketi,soksi, begi, madaftari na rula) vile vile na ada ya mwaka mzima kwa wanafunzi hawa. Zifuatazo ni baadhi ya picha za tukio hilo. 

Habari hii inapatikana kwa ufupi sana kupitia www.kitongoni.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mungu awabariki sana muendelee na moyo huo huo.

    ReplyDelete
  2. Mungu awabariki. Ni mfano mzuri sana kwa hao watoto na jamii kwa ujumla.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...