Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson 

Na Mwandishi Maalum
Wakati viongozi wakuu  mbalimbali nchini Tanzania  wakisisitiza haja na umuhimu wa viongozi wa madhebu ya dini kuwa na utaratibu wa kukutana mara kwa mara. Umoja wa Mataifa nao kwa upande wake  unaeleza kwamba ni kwa  njia ya  mazungumzo  migogoro ya dini inaweza kuepukika.
 Kauli hiyo ya Umoja wa Mataifa,  umetolewa na  Jan Eliasson,Nabu Katibu Mkuu wa  chombo hicho ya kimataifa ,  wakati wa  tukio maalum  la Muungano  kwaajili ya utamaduni wa Amani kwa njia ya  maelewano ya  madhehebu ya dini. Tukio ambalo limefanyika mwishoni mwa wiki hapa umoja wa mataifa likiwahusisha  wawakilishi kutoka  dini mbalimbali, vyama visivyo vya kiserikali na mabalozi.
“Migogoro mingi inayoendelea  hivi sasa duniani,  ni migogoro ya kidini. Mazungumzo baina ya imani mbalimbali yanaweza kusaidia kusuluhisha migogoro hii.  Tunaweza kupambana na chuki kwa njia ya mazungumzo   ili kujenga maelewano   na kujenga daraja la maisha bora kwa jamii zetu”.Akasema  Naibu Katibu Mkuu
Na kuongeza kuwa, dini zote zimekuwa  mstari wa mbele katika juhudi si tu za kuhimiza amani na upendo, bali hata katika miradi ya  kuwasaidia watu maskini kwa kutoa huduma  kama vile za afya, na kuwasaidia vijana.
 Hata hivyo akaonya kwamba, siasa kali za  kidini zimekuwa chimbuko la uharibifu wa kudumu na  mateso  katika jamii.
Na kwa sababu hiyo akasisitiza kutoachiwa kwa vikundi vya dini vyenye misimamo mikali  kuharibu na kuvuruga amani  na maendeleo na kazi nzuri inayofanywa na madhehebu ya dini .

 “Hatuwezi kuruhusu kundi dogo la watu wenye misimamo mikali  kuharibu kazi nzuri zinazofanywa na  jumuia za kidini kwa waumini wao duniani kote” akahimiza Bw. Eliasson
Akaelezea  wasi wasi wake kuhusu vijana kutumiwa  na vikundi vyenye misimamo mikali kueneza  kampeni za chuki na  vurugu kwa ahadi za kupata dhawabu au wokovu ili wao watimize malengo yao.
“Kwa kawaida  vijana wana nguvu.  Tunapashwa  kutafuta   njia nzuri na sahihi za kuwafanya wazitumie nvugu  zao kuboresha maisha yao” akasisitiza Naibu Katibu Mkuu.
Naye  Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw. Vuk Jeremic kwa  upande wake alisema  Umoja wa Mataifa unaweza  kufaidika sana  kama viongozi wote wa dini watajihusisha na kufanya kazi kwa moja ili kuleta amani. Huku akiutaka  Umoja huo kuogeza kasi ya kushirikiana na madhehebu ya dini.
“ Hebu basi  na turejee na kukumbatia wito unaotolewa na imani zetu, wito wa kuwasaidia watu wengine wenye matatizo, wito wa kuheshimiana wenyewe kwa  wenyewe,ikiwa  ni pamoja na  uhuru wa kuabudu wakati wowote na mahali popote bila ya kujali tofauti zetu za imani”.
Rais huyo wa Baraza Kuu akasema kila mtu anawajibu wa kuwasiliana na mwenzake na kusahau yaliyopitia na kuonya kwamba kama vyanzo vilivyopita  vya migogoro ya kidini vitaendelea kukumbushiwa mara kwa mara, kuna hatari kubwa ya kuitumbukiza dunia katika  machafuko ya kutisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hakuna migogoro ya kidini. Ingekuwepo, watu wangekuwa wanagombania usahihi wa imani zao na hapo kungekuwa na migogoro zaidi ndani dini zenyewe. Kilichopo ni Biashara tu, migogoro ina faida kubwa kwa baadhi ya vyama, taasisi za kiraia, kidini au watu binafsi. Ujinga wa waumini unatumika tu. Ndiyo, dini imegeuka biashara na migogoro ni kama matangazo ya hizo biashara.

    ReplyDelete
  2. Hatuwaamini hawa wazungu. Ndo maana walimuondoa Dr. Asha Rose Migiro. Wanataka waafrika tuamini kuwa migogoro ya kidini ndo tatizo badala ya "unequal distribution of wealth". Wao wazungu wanaendelea kutunyonya. Matabaka ya kiuchumi ndo yanaleta migogoro wala si kitu kingine na wao hili hawataki kulikubali ili waendelee kututawala. Wanajifanya kuwa vurugu za Afrika zinasababishwa na udini na ukabila. Kwani udini na ukabila unaletwa na nini kama si umasikini unaochangiwa kwa kiwango kikubwa na wazungu wenyewe? Mdau-CA, USA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...