Naibu mkuu wa pili wa Idhaa za Kiswahili wa DW, Josephat Charo. akimpa mkono wa heri kwa furaha Mtangazaji Stumai George baada ya kumaliza muda wake wa mwaka mmoja kuhudumu kama mtangazaji DW.
  Stumai George akipewa mazagazaga  na kulambishwa nondo ya bye bye  mama lakini uwe unakumbuka DW na Naibu mkuu wa pili wa Idhaa za Kiswahili wa DW, Josephat Charo mjini Bonn.
 Wafanyakazi wa DW katika hafla fupi ya kwa heri ya kuonana  Stumai George ambae anarudi Star TV Dar es Salaam.
Wafanyakayi wa DW na Kicheko kinachoashiria dhahiri kwamba Stumai George pamoja na kuondoka lakini mwenzao wa dhati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. WANZAAGWA KUTOKA NCHI GANI KURUDI TZ?

    ReplyDelete
  2. Mdau huyo Mtangazaji anaagwa kutoka nchini Ujerumani kurudi Tanzania.

    ReplyDelete
  3. Stumai George baada ya mwaka mmoja wa kula ma-Hamburg na junk foods sasa karibu tanzania ili ule:

    1-Ugali wa dona kwa mbaazi kavu,
    2-Ugali kwa matembele,
    3-Dona kwa Kisamvu mchanganyiko na kunde mbichi,
    4-Ugali kwa Dagaa la Kigoma,
    5-Mchanyato wa maboga, maharage mabichi na viazi kwa maziwa ya mtindi,
    6-Wali chuku chuku kwa samaki ndobe,
    7-Makande kwa Kachumbari(Biriani Pori)

    Nadhani Menu hiyo hapo juu itawajaza mate ya makoo wa Majuu au siyo?

    ReplyDelete
  4. hahahaha mdau watatu,

    Bibie Mtangazaji baada ya miziki ya kujiandaa kulala, hadi miziki ya wakati wa kula chakula ukiwa huko Majuu karibu Tanzania:

    -ucheze lizombe,-Kingoni.
    -echeze mdumange,-Kisambaa.
    -ucheze ndalandala,-Kimatumbi.
    -ucheze tokomile,-Kindengereko.
    -ucheze behobeho,-Kikwele.
    -ucheze mbeta,-Kiluguru.
    -ucheze mganda,-Kinyasa/Kiyao.

    !!!!!!!

    ReplyDelete
  5. DW msitupe jongoo na mti wake,

    Mtowe na mialiko ya mara kwa mara ili mdau mtangazaji abadilishane nanyi ujuzi na maendeleo, msibane kwa sana sasa...sio mara ohhh, Bajeti kutoka Bungeni Bundestag-Berlin safari hii hakuna fungu la kutosha!...mara ohhh, matumizi ya wageni wa nje yamepunguzwa!

    Wabaki hao Ubalozi pekee hapa Dar na sio ninyi tena!

    ReplyDelete
  6. mbona simuoni hapo Abuubakar Liongo...mzee wa yaliojiri?

    ReplyDelete
  7. Jirupue au kama ulikuwa na akili ulikuwa utafute dume likuzalishe. Rudi mama mkataa kwao mchawi.

    ReplyDelete
  8. Haaaaa umeniu na hiyo menu yako,,,1
    basi ujue majuu tena hapa Ujeru' kumejaa ma-Afro shop kibao....kambale...sato...mchicha...bamia, ngogwe vimejaa kwa wingi....Utumbo fresssh...alafu juzi nimepika kongoro!1 menu ya leo kuna mkia mzima wa n'gombe hapa sasa sijui kama nitamaliza. Unakula ukiwa bongo ndo unazidisha hasira ya kuzichanga...haaaaaa

    ReplyDelete
  9. Mate ya kinywa bwana siyo ya makoo, koo haliweki mate ya kutamanisha vyakula, huweka ya kikohozi. Ila siyo siri, kweli hiyo MENU inatamanisha.

    ReplyDelete
  10. Mbona simuoni cheupe a.k.a WHITE?
    Au alienda K.F.C? bwahahaaa!
    Au anahuzunika Stumai kuondoka?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...