Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Dianna Melrose. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ofisini kwa Mhe. Membe, tarehe 27 Februari, 2013.
Mhe. Waziri Membe akionesha Nakala hizo mara baada ya kuzipokea.
Mhe. Membe akizungumza na Mhe. Melrose masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uingereza mara baada ya kupokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi huyo.
Mhe. Balozi Melrose akimsikiliza Mhe. Membe wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Balozi Dora Msechu (wa pili kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bi. Zainab Angovi (kushoto), Afisa katika Idara ya Ulaya na Amerika.
Mhe. Membe akimsikiliza Balozi Melrose alipokuwa akifafanua masuala mbalimbal ya ushirikiano.
Mhe. Membe akiagana na Mhe. Balozi Melrose mara baada ya mazungumzo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...