Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh Edward Lowassa leo amezungumza mambo kadhaa ambayo kimsingi yameitikisa na kuishtua jamii kwa kiasi kikubwa,amezungumzia suala la Elimu na mustakabali wake unavyokwenda hapa nchini,kama vile haitoshi akazungumzia suala la la baadhi ya watu kuleta mitafaruku ndani ya jamii kiasi hata ya kusababisha uvunjifu wa amani katika nchi yetu,Bofya video hizo juu na chini kumsikiliza Mh Lowassa alichozungumza kwa kina mapema leo kwenye moja ya ofisi zake zilizopo Mikocheni,Jijini Dar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Amani ni nzuri ila nadhani watanzania hatujui maana ya amani. Nchi kama Rwanda na Burundi ndio wanaoweza kueleza maana ya amani kwa uhalisia wake sio ni kama tuna theory ya amani ila practical wenzetu Rwanda, Burundi na South Africa au Middle East wanaweza kukueleza Practical issue with regard to Amani

    ReplyDelete
  2. Wanasiasa wetu uwezo wao wa kufikiri unaishia kwenye tume. Hili la lemu tafiti nyingi ziliza fanyika chakufanya wahusika wafungie makablasha ya taasisi ya elimu na watakuta mapendekezo ya kutosha nini kifanyike kuhusu helimu yetu. Pili mass failure ya form four ni kutokana na project ya shule za kata. Hizi shule zifute.

    ReplyDelete
  3. Kwa sasa tunaye rais. Hakuna haja ya kufanya kampeni kwa sasa. Maana kila jambo lazima Lowasa atoe comment. Sasa wananchi tunashindwa kuelewa kwa nini anafanya hivyo?

    ReplyDelete
  4. Mzee kaongea maneno mazito yenye busara kubwa kwa wabongo...wenye masikio na wasikie..hakuingia kwenye siasa wala nn just point tupu.
    mdau wa kwa mama-UK

    ReplyDelete
  5. Tatizo ni Moja Mheshimiwa Lowassa. Umetoa maneno ya busara sana lakini sisi wananchi tuna wasiwasi na hizi amani ambazo wachache wamezitumia kutunyonya kwa kujinufaisha. Sasa tuambieni kuwa amani imemsaidiaje mtu wa kijijini na wamachinga? Mimi nashindwa kuelewa kuwa hii amani yetu imetusaidia nini zaidi ya wachache kula kwa ulaini na hatuwafanyi kitu.

    ReplyDelete
  6. vyama ndio chanzo kikubwa cha uvunjifu wa amani hapa nchini kwetu....wanawadanganya watu kiasi kwamba watu wanaingiwa na hasira na kufanya maamuzi mabaya na pili huhamasisha vurugu.

    ReplyDelete
  7. mimi sikubaliani na huyu bwana hakuna haja ya kwenda kwenye vyombo vya habari kumshauri Rais nini cha kufanya hiyo si kazi yake,Rais ana watu waonalipwa kufanya kazi ya ushauri. Pili TZ viongozi wanaihujumu nchi kwa hali ya juu sana ndiyo maana hakuna maendeleo hata ya elimu. viongozi wengi wanajivika ngozi ya kondoo kumbe ni mbwa mwitu ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa.RIP baba wa Taifa

    ReplyDelete
  8. Suala uvunjifu wa amani haswa kupitia vikundi vya waumini wa dini,vinatokana na waumini kupotoshwa na baadhi ya taarifa zisizo sahii zinazo enezwa na wazushi.
    Au pengine ni taarifa ambazo serikali inazisikia na kuzipuuza mpaka zinafika kuleta uvunjifu wa amani.
    Kingine ni watendaji kaza katika sekta za umma wamekua wameweka dini zao mbele kuliko wajibu na kanunni za utumishi katika jamii. kwenye ofisi ya serikali mtu kaweka nembo au picha inayoonyesha yeye dini gani? unachokitegemea nini? kama sio choko choko

    ReplyDelete
  9. "wale wanaosahau historia yao kuna uhakika watarudia makosa yao". Para-phrasing. Tuusisahau ndugu zangu kwamba hili janga la elimu limechangiwa sana na Mh. huyu aliposukuma sekondari za kata. Alishauriwa na watalaam kwamba iwe program ya mda mrefu na iambatane na uwekezaji (resources) kwenye MAABARA na WALIMU WA KUTOSHA NA WENYE MISHAHARA NA MAZINGIRA MAZURI YA KUISHI HASWA VIJIJINI hakukubali kwani kwa miaka ile 2005-2007 hizi shule ziliongeza umaarufu wake, wa chama madarakani na wa serikali. Now the chickens are coming home to roost! si za kata tu hata za zamani zinasahaulika. Siasa NOT Utaalam umetufikisha hapa. Tubadilike kwa kuanza kusema ukweli chanzo cha matatizo na hapo tupatie dawa na turekebishe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...