Mrisho
Mpoto akiigiza kama FALSTAFF na kulia ni Bw Ogutu Mulaya, alie tafasiri mchezo
huu kwa Kiswahili, akicheza kama Bi Quickly.
Mrisho
Mpoto akiwa na waigizaji wenzake kutoka Kenya ambao waliigiza kama WANAWAKE WA
HERI WA WINSA wakionesha umahiri wao
katika Ukumbi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.
Kulia
kabisa ni Bw Ogutu Mulaya, alie tafasiri mchezo huo kwa Kiswahili, akiigiza na
wenzake huku akiwa kwenye husika nyingine.
Mrisho Mpoto ni moja kati ya wasanii
wakubwa wa Muziki na Maigizo ya Jukwani hapa nchini. Michezo hii ya jukwaani ambayo
ni adimu na adhimu sana hapa nchini kutokana na umakini na utaalaam mkubwa unao
hitajika katika uandishi, uongozaji na hata uchezaji jukwaani.
Hapa nchini kuna wasanii wachache wenye
uwezo wa kutimiza hatua zote za maandalizi ya mchezo wa jukwaani. Tumekuwa
tukishuhudia wataalam walio pikwa kutoka
Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo na wale wa Chuo kikuu cha Mlimani katika
Idara ya Sanaa na Maonesho na Chuo kikuu Huria wakishughulika sana na tasnia
hii.
Baada ya kuona Tasnia hii inasua sua, Bwana
Mrisho Mpoto aliamua kwa dhati kurudisha heshima ya michezo hiyo kwa kuishawishi
kampuni inayo jishughulisha na Maonesho ya Jukwaani ya nchini Kenya Kuuleta
mchezo ulio jipatia umaarufu mkubwa kwenye nchi mbali mbali ulimwenguni na hata
kupata heshima ya nyota tano nchini Uingereza ambapo Mrisho yeye mwenyewe
akiucheza mchezo huo kama mhusika mkuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...