ANKO HABARI,

NAOMBA UNISAIDIE KUIRUSHA HII, 
NIMEPANDA DALADALA ASUBUHI HII KUTOKEA KONGOWE KWENDA TANDIKA, SIKUPATA KITI. NILIMWOMBA MWANAFUNZI MMOJA ANISHIKIE MFUKO WANGU UKIWA NA VITABU. NILIPOFIKA MTONI KWA AZIZI ALI, NIKASHUKA NA KUSAHAU KUUCHUKUA MFUKO HUO,NILIPOHAMAKI GARI TAYARI LIMESHAONDOKA NA BAHATI MBAYA ZAIDI KONDA HAKUTOA TIKETI. 
MWANAFUNZI ALIVAA SARE KAMA YA WAILES SEKONDARI. NIMEENDA PALE HAKUWEZA KUPATIKANA. 

VITABU VIKO VITANO:
1.FROM GOOD TO GREAT
2.BUILT TO LAST
3.EXECUTION
4.STRATEGY  NA CHA TANO SIKIKUMBUKI MAANA NILIVICHUKUA NI VYA MTU. NI VITABU VYA LEADERSHIP,NDANI VIMEANDIKWA E.MSANGI.

NAOMBA KAMA MWANAFUNZI HUYO ATAKUWA HANA NAMNA YA KUNIPATA BASI AWASILIANE NAMI KWA NAMBA 0755877827 AU0767626929

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Kwanza pole kwa kupoteza vitu vyamtu. na huo ni ujinga mkubwa kila siku hayo mambo yanaongelewa. huwezi kumpa kitu mtu hajui ndani kuna nini na ni mwanafunzi. ati akushikie hayo nimakosa yako. watu wanatapeliwa namna hiyo ndani ya madaladala kilasiku. nishawahi kusoma humuhumu.na wewe unafanya tena makosa. tena wewe unapaswa ulipe haraka dhamana ya watu.

    ReplyDelete
  2. Hiyo sio uzembe bali ni kupitiwa au teseme ubinaadamu.

    Jamaa ameomba asaidiwe kubeba huku akiwa hajapata kiti ndani ya basi, hivyo aloposhuka hakukumbuka kama alipanda na mzigo.

    Pole sana ndugu E.Msangi!

    ReplyDelete
  3. wewe mtoa maoni wa kwanza,ninashaka kama unaongea ukiwa hapa nchini,mazingira ya usafiri wa hapa bongo ndiyo yanatufanya tuombane misaada ya kubebeana mizigo ndani ya daladala,inafikia hata wakati watu wazima wanapitia madirishani,hapa si ujinga ni ubinadamu tu,ingekuwa ujinga michuzi issa asingekubari kuweka jambo la ujinga hapa,hii ni blog ya jamii si yakijinga kama unavyofikiria.
    Ninashaka kubwa sana na uelewa wako wa mambo nakuomba sana usiwe unakurupuka kutoa maoni bila kuyatafakari,huyu mtu kapoteza vitu vyake,anaomba msaada kwa jamii imsaidie kama inawezekana na harazimishi mtu ,wewe unamwona mjinga. Kama ulivyomwita mwenzio mjinga kwa kuomba msaada,kunasiku litakupata jambo na utahitaji msaada kwa watu ndipo utakapo jua uliyoyaongea.Nakuombea maisha marefu yenye mafanikio sana ili uendelee kuita watu wajinga.AMEN

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...