Flashback Desemba 14, 2008: Mgombea Urais wa TFF Jamal Malinzi (shoto) na mgombea Umakamu wa Rais wa TFF Ramadhani Nasib wakitafakari nje ya ukumbi wa NSSF Waterfront House jijini Dar es salaam kabla ya uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo kuanza. Mshindi wa Urais aliibuka Sir Leodegar Chilla Tenga na Nasibu alishinda Umakamu wa Rais. Kupata habari zingine za siku hiyo BOFYA HAPA.
--------------------------------------------------------------
Ndugu zangu, kupitia vyombo vyenu vya habari ninaomba niueleze umma wa watanzania,hususani wadau wa mpira wa miguu,yafuatayo kuhusu kuenguliwa kwangu.
Awali ya yote nieleze kusikitishwa kwangu na maamuzi yaliyotolewa na kamati ya rufaa ya TFF ya kuniengua kugombea urais wa TFF.Sikubaliani na maamuzi haya.
Katika kuniengua kamati ya rufaa ya uchaguzi ya TFF imetoa sababu mbili (nanukuu magazeti ya jana tarehe 12/02/2013 maana hadi leo sijakabidhiwa barua ya kuenguliwa).
Mwachie kwanza Sir Leodgar Tenga malize muhula wake mpya maana kazi aliyofanya ni kubwa na Ndugu Jamal uzoefu wa kuenguliwa utumike ktk kuboresha uchaguzi mwingine utapokuja.
ReplyDelete