Kundi la Nyumbu madume wakiwa wamejikusanya pamoja Serengeti wakiangalia watoto wao wanavyofurahia mandhari ya Serengeti.
======= ====== ===
Watalii wafurika
Serengeti kushuhudia tukio la Nyumbu kuzaliana
Zaidi ya Watalii
16,500 kutoka mataifa mbalimbali ulimwenguni miongoni mwao wakiwemo Watanzania
5,800 wamefurika katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya kushuhudia
tukio adimu linalohusisha Nyumbu wapatao elfu nane (8,000) kuzaliwa kila siku.
Mwezi Februari kila
mwaka ndipo msafara wa Nyumbu hufika katika eneo la kusini mwa Serengeti kwa
ajili ya kuzaliana. Miongoni mwa wageni waliofika Serengeti mwaka huu
kushuhudia tukio hili muhimu ni pamoja na watafiti wa wanyamapori na
wanazoolojia wanasayansi maarufu sana ulimwenguni.
Msimu wa Kuzaliana
katika Serengeti ni tukio la kipekee ambapo ni Serengeti pekee duniani ambapo
wanyama hawa huzaliana kwa pamoja katika mzunguko wao wa mwaka mzima.
Msimu huu wa
kuzaliana utadumu kwa muda wiki sita ambapo hadi kukamilika kwake inatarajiwa
kuwa ndama wapatao 500,000 watakuwa wamezaliwa katika eneo la Serengeti ambayo
ni hifadhi ya pili kwa ukubwa nchini Tanzania.Kinchosisimua zaidi katika tukio
hili ni pale ambapo nyumbu hawahitaji kulala chini kwa ajili ya kuzaa bali
tukio hili huendelea huku Nyumbu akiwa anaendelea kutembea na kula malisho ya
majani hifadhini.
Cha kipekee zaidi ni
pale ndama aliyezaliwa mara tu akishazaliwa, humchukua kati ya dakika mbili
hadi tatu kuanza kurukaruka na kumfuata mama yake kwa kasi kubwa.
Hata hivyo miongoni
mwa ndama hawa wanaozaliwa kipindi hiki, wengi wao wapo hatarini kuliwa na
wanyama wakali wanaowawinda kwa hamu kubwa kwa ajili ya kujipatia chakula.
Wanyama hawa maarufu kwa kuwinda ndama hawa ni pamoja na fisi wanaofikia 7,500
pamoja na simba zaidi ya 3,000 ambao wote hukodolea macho tukio hili kwa nia ya
kujipatia mlo wao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...