Waziri
wa Nishati na Madini wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Dk Sospeter
Muhongo, anatarajia kufanya ziara ya kikazi nchini Uingereza kuanzia tarehe 25
hadi 28 Februari 2013.
Akiwa
London Mhe. Waziri angependa kukutana na Watanzania waishio Uingereza
kuzungumzia maendeleo ya sekta ya nishati na madini Tanzania na pia
kubadilishana nao mawazo kuhusu maendeleo ya sekta hiyo.
Ubalozi
wa Tanzania, London unapenda kuwakaribisha watanzania siku ya Jumanne tarehe
26, Februari 2013, Ubalozini saa 11
Jioni. Anuani ya Ubalozi ni 3 Stratford Place, W1C 1AS, London
Wote
mnakaribishwa.



Wandugu mliopo UK hiyo ni nafasi muafaka.
ReplyDeleteMwelezeni Mhe. kuwa haya mambo mawili (2) hapo chini ni muhimu kurekebishwa ili twende na wakati.
Kwa kuwa dhamira kubwa ni kuleta Tija ktk Sekta ya Nishati Serikali kupata faida pia na kuwafikia Wananchi kwa manufaa.
1.Masoko ya Hisa kuwa wazi kwa kufungua,
(i)T-Bonds and T-Bills (Dhamana za madeni kuweza kuwekezwa na wananchi wa kawaida badala ya Taasisi peke yake kama ilivyo sasa)
(ii)Kuondoa Limit ya ununuzi wa Hisa usizidi 60% ktk Masoko, na pia kuwaruhusu Wageni (na Waliopo nje ya nchi kama ninyi Madiaspora) kuwekeza au kuwa Wadau ktk Soko huku Usimamizi makini ukiwepo.
(iii)Kulifungua Soko liweze kufanya Biashara na nchi za nje, Cross border Trading Links, na kupanua wigo wake wa ufanisi ili kuakisi Mitaji ya nje zaidi.
(iv)Kubadili Sheria zinazobana Uwekezaji na hasa kuingiza Sheria na kanuni za Kibiashara ktk Sekta ya Nishati (Energy Sector Commercial Laws)
(v)Majukwa ya Uwekezaji (Investment Portifolio) yawe wazi kuruhusiwa kwa watu wananchi wa kawaida.
KAMA INAVYOONEKANA SERIKALI INATAFUTA US$ 10 BILLION ILI KUPATA UWEZO WA KUJENGA MIUNDO MBINU NA VIWANDA VYA BIDHAA ZA GESI, WAKATI FEDHA KAMA HIYO INGEPATIKANA KWA NJIA KAMA HIZO HAPO JUU (i) na (ii) KUTOKA VYANZO VYA HUMU HUMU NCHINI BADLA YA KUKOPA KWA RIBA YA JUU KWENYE VYOMBO VYA NJE YA NCHI.
2.Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (Social Security) ndio njia muafaka kuwezesha faida ya Rasilimali kuwafikia Wananchi na kuondoa Umasikini nchini kwa kuanzisha Dhamana za Huru (Sovereign Bond), kama jinsi nchi za Norway,Oman na United Arab Emirates (UAE) zilivyo fanikiwa kuweka jamii zao nje ya Umasikini kwa Rasilimali za Nishati walizonazo (Oil and Gas,Energy Sector).
Kama tunavyoona sasa Mifuko kama NSSF,GEPF na mingine imeweza kukuza wigo wake kuwafikia hata wananchi wa kawaida.
Hivi kama mawaziri wanakwenda kuonana na watanzania katika baadhi ya nchi hasa Uk. Hizi balozi zetu na wafanyakazi wake wanafanya nini kushindwa kuwakilisha serikali na nchi huko nje.
ReplyDeleteHuyu mh. Prof mihongo anachoma kodi zetu kwenda kutalii London kwa kisingizio cha ajabu kabisa. Hizi ni kazi za mabalozi na si mawaziri kuacha afisi dar kwenda nje.
Hiki ni kichekesho...kama ni nishati kwa nini asiende angalau Sauzi Afrika, korea, au UAE ambao wako safi tuuuu.....