Hatimaye Ndugu Jamaa na Marafiki waishio Jijini Dar es Salaam pamoja na Wafanyakazi wenzake na Marehemu Grace Mathew Chao leo wametoa heshima za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Mpendwa wao Grace katika zoezi lililofanyika Katika Hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salaam ambako mauti yalimkuta Februari 17, 2013. Grace Chao alizaliwa Desemba 13, 1985.

Mwili wa Grace ulisafirishwa kuelekea Mazimbu Mkoani Morogoro ili kuwapa fursa wana jamii ya Mazimbu na Mzumbe ambako marehemu alizaliwa na kuishi zoezi ambalo litafanyika kesho Jumatano kabla ya Msafara kuelekea Marangu kwa mazishi. 

 Vijana mbalimbali wa Kundi la Home Sweet Home – Kimzumbe Mzumbe waishio jijini Dar es Salaam kwa shughuli za kazi na masomo walijitokeza kuuaga mwili wa Mwana Mzumbe mwenzao.
 Mama wa Marehemu Grace (kushoto) akiwa na mwana familia mwingine wakati wa zoezi hilo leo.


Ilikuwa ni majonzi sana katika tukio hili, kwa Vijana mbalimbali wa Kundi la Home Sweet Home – Kimzumbe Mzumbe waishio jijini Dar es Salaam walijitokeza kuuaga mwili wa Mwana Mzumbe mwenzao.

 Wafanyakazi wa CRDB Bank waliita kutoa heshima kwa Mwili wa Mfanyakazi mwenzao.
 Vijana wa Mzumbe Wengi sana walijitokeza kumuaga Grace katika safari yake hiyo ya Mwisho.
Marafiki na vijana wa Mzumbe wakimfariji kaka wa Marehemu Edwin Ndesamburo Chao (kulia) kufuatia msiba wa dada yake.
Picha na Father Kidevu blog.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...