Pichani ni Baadhi ya Maofisa wa Ofisi Ndogo ya Bunge,wakimsaidia kwa kumbeba Mbunge wa Chambani,Bwa.SalimHemed Khamis,mara baada ya kuanguka ghafla hapo jana jijini Dar akiwa katika vikao vya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu ya haraka.
=======  ======  ======
Habari  zilizoifikia Globu ya Jamii hivi punde inaelezwa kuwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Chambani-Pemba, Salim Hemed Khamis,ambaye hapo jana alianguka ghafla jijini Dar Es Salaam alipokuwa akihudhuria vikao vya kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu, amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali hiyo ya Taifa ya Muhimbili,aidha chanzo cha habari hizi kimeongeza kuwa taratibu za kuusafirisha mwili wa Marehemu kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.Tutazidi kuwafahamisha zaidi kadiri ya habari zitakavyokuwa zikiingia.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema Peponi-Amin 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. inna lillah wa inna illayhi rajium, Muumba amweke katika kundi la waja wema

    ReplyDelete
  2. Mungu amlaze pema Langu ni hili Yaani ni aibu kUBWA TANZANIA basi tunasihdwa hata kuwa na gari la kubebea wagonjwa katika offisi za bunge? au hata daktari mmoja maeneo muhimu hayo.

    Aaama kweli

    ReplyDelete
  3. natoa mkono wa pole kwa wafiwa na taifa kwa jumla,pia ningeomba kuwe na mpango maalum wa kuwapima wabunge wote afya zao uelewa wangu si wao tu majuzi nilifiwa na mjoba wangu amabe alikuwa ana bllod pressure lakini hamna aliyekuwa akijua pamoja na yeye mwenyewe tulijua baada ya kuanguka na baadae kufa.
    kwa tanzania ni jambo la kawaida ndio maana tuna ule msemo wetu wa kawaida "kafa ghafla" hamna hiyo ni uchunguzi wa kawaida wa afya ili tuweze kutumia kinga.
    mungu amlaze mahala pema amin.
    mdau.
    dodoma.

    ReplyDelete
  4. Ameen @anonymous 1....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...