Bondia Prince Immanuel Naidjala

Bondia wa Namibia na bingwa mara nne wa WBO Africa, Immanuel "Prince" Naidjala anakwenda matawi ya juu baada ya Shirikisho la Ngumi la Kimataifa kumpa nafasi ya kugombea mkanda wa IBF wa mabara.  

Prince Naidjala ambaye amewapiga mabondia kibao kutoka nchi nyingi za kiafrika ikiwamo Tanzania anakutana na bingwa wa ngumi kutoka Botswana Leslie Sekotswe katika kindumbwe ndumbwe cha kuwania mkanda huo wa IBF wa mabara (IBF Intercontinental title).                  
 
Mpambanio huo utafanyika tarehe 20 Machi katika ukumbi wa Casino ya Country Resort Club jijini Windhoek, Namibia chini ya promota Nestor Tobias wa kampuni ya Sunshine Boxing Productions iliyoko nchini Namibia.

Naidjala ana rekodi ya mapambano zaidi ya 16 na ameshinda yote mengi 10 kati ya hayo ameshinda kwa KO wakati Leslie Sekotse ana rekodi ya mapambano 11 na ameshinda 8 kwa Ko na kutoka sare moja.

Naidjala ni kati ya mabondia wanaopewa nafasi kubwa sana kutoka Afrika kuwa mabingwa wa dunia. Kama akishinda taji hili, atakuwa bondia mwenye hadhi kubwa sana kutokea Namibia tangu enzi za bondia Harry Simon ambaye alitingisha Afrika miaka ya 90.

Nalo Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limemuingiza Naidjala katika orodha ya mabondia walio kwenye viwango vya mabara na hana kizuizi chochote cha kumfanya agombee ubingwa huo!

ISSUED BY:
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...