Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha Mitindo House,Bi.Khadija Mwanamboka wakwanza kutoka kushoto waliosimama,akiwapa muuongozo baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha rasiliamali watu cha Vodacom waliotembelea kituo hicho kutoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali vywenye thamani ya shilingi milioni mbili,katika mwendelezo wa kampeni ya pamoja na Vodacom inayoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo,Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Afisa ustawi wa jamii wa Vodacom Tanzania,Bw.Ndehagati Biduga,akiwafundisha jambo watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Mitindo House mara baada ya hafla fupi ya kukabidhi msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi milioni mbili kupia kampeni ya Pamoja na Vodacom inayoendelea kufanywa na wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Maendeleo rasilimali watu wa Vodacom Tanzania,Bw. Conrad Msoma, akianalia moja ya michoro aliechora mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Mitindo House,wafanayakazi wa kitengo cha rasiliamali watu cha Vodacom walitembelea kituo hicho kutoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali wenye thamani ya shilingi milioni mbili,katika mwendelezo wa kampeni ya pamoja na Vodacom inayoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo,Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Afisa ustawi wa jamii wa Vodacom Tanzania,Bw.Ndehagati Biduga,akimkabidhi mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Mitindo House kilichopo jijini Dar es Salaam,msaada wa mchele,msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni mbili ulitolewa na Vodacom Tanzania kupitia kampeni yake ya pamoja na Vodacom inayoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo, hivi karibuni.
Mkuu wa kitengo cha Maendeleo rasilimali watu wa Vodacom Tanzania,Bw. Conrad Msoma, akimkabidhi mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Mitindo House,Galoni ya mafuta ya kula kama sehemu ya msaada wenye thamani ya shilingi milioni mbili kutoka Vodacom Tanzania kupitia kampeni yake ya pamoja na Vodacom inayoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo,Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...