Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akizungumza na  aliyekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Mawaziri wa Japan, Bw.Osamu Fujimura alipofika na ujumbe wake Ofisini kwa Mhe. Waziri leo ambapo walizungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Japan ikiwemo maandalizi ya Mkutano wa Tano unaohusu Ushirikiano kati ya Japan na Afrika (TICAD V) utakaofanyika nchini humo mwezi Juni 2013.
Mhe. Membe akiendelea na mazungumzo huku ujumbe kutoka Japan ukimsikiliza.
Mhe. Membe akimsikiliza Bw. Fujimura wakati wa  mazungumzo yao.
Mhe. Masaki Okada (kulia), Balozi wa Tanzania hapa nchini akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati ujumbe kutoka Japan ulipomtembelea Mhe. Membe ofisini kwake. Wengine katika picha ni Balozi Mbelwa Kairuki (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Khatib Makenga, Afisa katika Idara hiyo.
Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Bw. na Bibi Fujimura (kushoto) na Mhe. Masaki Okada (kulia), Balozi wa Japan hapa nchini mara baada ya mazungumzo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...