Ndugu waTanzania wenzetu,

Tunayo furaha kuwaalika kuhudhuria mkutano kati ya Balozi wetu mpya (Tanzanian Ambassador to the Kingdom of Belgium, the Kingdom of Netherlands, the Grand Duchy of Luxembourg, the European Union and International Organisations based in the BENELUX region)Mhe. Dr. Deodorus Kamala  na Watanzania waishio Uholanzi.

Mkutano huu umeandaliwa na Ubalozi pamoja na Kamati ya Umoja wa waTanzania hapa Uholanzi (TANE). 

Siku na Muda wa Mkutano:
Jumamosi, 16 Machi, 2013; Kuanzia saa  8.00 Mchana

Mahala:
Institute for Social Studies
Kortenaerkade 12, 2518 AX, Den Haag
Dorus Hall
Zuid-Holland, Nederland.

Karibuni nyote kwa kujali muda uliopangwa.

Wenu,

Kweba Bulemo
Mwenyekiti, TANE

Kny. Kamati ya Utendaji.

 TANBIHI:

Kufika eneo la mkutano, unaweza kutumia Bus namba 22 na 24 (Den Haag Central Station), au Tram namba 1 au 17 (Den Haag HS)

Shuka kituo cha Mauritskade. Ni mwendo wa dakika tatu mpaka ISS Dorus Hall.
Chuo cha ISS kipo opposite na Den Haag Hilton Hotel.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...