Balozi Rajabu Gamaha, Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika mazungumzo na Balozi Roberto Azevedo, Mwakilishi wa Serikali ya Brazil katika Shirika la Biashara Duniani (WTO) lenye Makao yake Makuu mjini Geneva, Uswisi, alipofika Wizarani tarehe 2 Machi, 2013 kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe maalum. Balozi Azevedo pia ni mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo.
Mhe. Balozi Azevedo akiwa na ujumbe aliufuatana nao  wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao. Kulia kwa Balozi Azevedo ni Mhe. Fransisco Carlos Luz, Balozi wa Brazil hapa nchini.
Balozi Gamaha akiendelea na mazungumzo na wageni wake.

Balozi Azevedo akiendelea na mazungumzo na Balozi Gamaha. Wengine katika picha ni Balozi Celestine Mushy (kushoto kwa Bal. Gamaha), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Lucas Mayenga (kulia), Afisa katika Idara hiyo.
Balozi Gamaha akifafanua jambo kwa Balozi Azevedo wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Fransisco Carlos Luz (wa kwanza kulia), Balozi wa Brazil hapa nchini pamoja na wajumbe wengine kutoka Brazil wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) alipozungumza nao
Wajumbe wote kwa pamoja wakimsikiliza Balozi Gamaha.
 

Balozi Gamaha akiagana na Balozi Azevedo mara baada ya mazungumzo yao.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Dr.Azevedo wa WTO kilichomleta ni kuiomba Tanzania Kura yetu ktk Uchaguzi huo.

    Tutaangalia kwa kuwa Mariam Mohamed wa Kenya ndugu zetu wa EAC alikuwa ktk UNEFPA ni pia Mgombea wa nafasi hiyo.

    ReplyDelete
  2. Juice kwenye mkutano ya nini? Mambo ya nje nao wamekuwa kama Ofisi ya tawala ya mikoa? Utaribu wa kimataifa toa maji ya kunywa sio juice! Maskini nje wanadhania wamewakirimu wageni hasa! Ama janja ya mabosi kupata makombo? Nilidhani hawa ndo wakongwe wa diplomasi ya mapokezi na vilaji na kuwa wangefahamu juisi wakati gani na maji ama chai wapi. Ajabu. Alafu twalia fomu four kufeli?

    ReplyDelete
  3. Anonymous wapili hapo juu unasomeka kama mtu mpuuzi puuzi vile!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...