Ubao wa Matokeo unavyosomeka mara baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Timu ya Taifa ya Morocco uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.
 Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Thomas Ulimwengu akiwatoka Golikipa na Beki wa Timu ya Taifa ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.Taifa Stars imeshinda Bao 3 - 1,mabao mawili yaliyotiwa kimiani na Mshambuliaji Machachari,Mbwana Samatha huku moja likifungwa na Thomas Ulimwengu.
Kiungo Mshambuliaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars),Shomari Kapombe akichuana vikali na Beki wa timu ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.
Lango la timu ya Morocco ilikuwa ni hatari muda wote wa mchezo.
 Kipa wa Timu ya Morocco akiusindikiza kwa Macho mpira ulioingia wavuni,baada ta kuigwa na Mchezaji Mbwana Samatta wa Taifa Stars.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Hongera Taifa Stars! ila hamkawii nanyi?

    ReplyDelete
  2. Big Up Stars! Hiyo ndio tunayotaka. Sasa fanyeni mkakati wa kushinda mechi ya marudiano. Mkishinda tu hiyo na kutoa sare na Gambia. Brazil ni yetu. Maana Ivory Coast lazima tu adinywe na Morocco, maana waarabu watataka kucheza Brazil hivyo watakaza uzi ili washinde.

    ReplyDelete

  3. SAFI SAAAAAAAAAANA WATANZANIA DUNIA NZIMA LEO TUNAFURAHA KWAUSHINDI HUU BIG UP KOCHA NA WACHEZAJI PAMOJA NA WASAHABIKI WOTE WALIOKUA UWANJANI KUTIA TIMU NGUVU. KWAKIWANGO HIKI TUTAFIKA MBALI SANA.

    MUNGU IBARIKI TANZANIA
    CHEF ISSA

    ReplyDelete
  4. tunaomba video ankali

    ReplyDelete
  5. Hongera sana Taifa Stars kwa ushindi huo.

    ReplyDelete
  6. Tatizo tukienda kwao marudiano 5 bila tuna pigwa.Tukaze hivyo hivyo. Naamini sisi wazuri kuliko San Marino

    ReplyDelete
  7. Michuzi tusaidie link ya kuona hiyo game replay please.

    ReplyDelete
  8. Hongera sana stars ili msipige ze pombe na starehe zisizo kikomo kazeni uzi tuko sambamba

    ReplyDelete
  9. MIE KWANZA KWA MATOKEO YA LEO YANATIA MOYO SANA ,NAWASIFU SANA KWANZA WACHEZAJI ,PIA NA WASHABIKI WOTE WALIOTIMBA KIWANJANI NA KUWAPA POLE WALIOKOSA GAME HII KWA SABABU ZISIZOZUILIKA!! HONGERA SANA KWANI TULISHACHOKA KUTAMBIWA NA NCHI ZA WATU KILA SIKU.NA NYIE MLIOKOMENT HAPA WOTE HONGERENI.

    ReplyDelete
  10. Funguwebsite hii utaweza ona magoli yote pamoja full match www.matchhighlight.com na mechi hii imeonyeshwa live leo online pia kwa kuangalia mechi yoyote duniali live online tembelea www.myp2p.eu

    Chef Issa

    ReplyDelete
  11. Pongezi Taifa Stars wembe huo huo uende kumnyoa Simba wa Maghreb tena nyumbani kwao.

    Nimeona vi-Bajaj vinaruhusiwa kuingia mpaka chini ya jukwaa la watazamaji ktk picha, je hakuna utaratibu mwingine ulio salama kwa mamia ya watazamaji maana mwendesha bajaj anaweza kubebesha kitu cha hatari bila kuelewa na kusababisha maafa kwa mamia ya watazamaji.

    Uongozi uangalie namna ya kufanya hali iwe ya usalama zaidi kwa kubuni njia ya kukabiliana na ugaidi unaoweza kufanya kwa halaiki ya watazamaji ikiwemo pamoja na walemavu pasipo kujua uhatari wa dunia ya sasa.
    Mdau
    Makini

    ReplyDelete
  12. hongera sn star ,game safi tukaze uzi tufike mbali,Hasna

    ReplyDelete
  13. wadau wenzangu kuona highlight link hii hapa http://www.matchhighlight.com/latest-goals/fifa/tanzania-3-1-morocco-wc-2014-qualif/

    ReplyDelete
  14. mi naomba kamati ya ufundi isibadilishwe, imefanya kazi nzuri. Naweza nikamwongezea na bibi yangu akawasaidia kidogo na bila malipo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...