Hotel ya kitalii ya Irente View and Cliff lodge yabambwa ikitumia umeme wa wizi mchana huu huko Lushoto,Mkoani Tanga. Hotel hii wameharibu mita kwa kuweka rezista kupunguza upimaji wa mita ili kujiwezesha kulipa kidogo sana. Hotel hii imekamatwa na kikosi maalum toka makao makuu ya Tanesco nchini kinachoongozwa na Meneja wa Huduma kwa Wateja wakubwa, Mhandisi Francis Maze. Mmiliki hajaweza kupatikana hivyo Tanesco wamekata umeme na kuondoka na mita na taratibu za kisheria zitafuata.Juu ni fundi kutoka Tanesco akikata umeme kwenye hotel hiyo.
Mhandisi Francis Maze wa pili toka kushoto, akimwelezea fundi wa hotel hiyo na maafisa wengine wa Tanesco kilichotokea.
Mita ya Irente View and Cliff lodge iliyoharibiwa kuruhusu wizi wa umeme.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hivi ni kuwakatia tuu au kushtakiwa na kufungwa jela? Huu ni usanii sasa..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...