Globu ya Jamii imepokea kwa mshituko mkubwa na simanzi taarifa
kuwa Bi Kidude katutoka. Tunatoa salaam za rambirambi kwa watu wote wa Zanzibar
pamoja na wa Bara waliomuenzi msanii huyu ambaye pamoja na umri wake mkubwa
aliendelea kutuliwaza kwa usanii wake jukwaani pamoja na matani na ucheshi usio
kikomo nje ya jukwaa. Kuna wachache wa aina yake Wallahi..
Akiwa ni mmoja wa wasanii nguli Bara na Visiwani, Bi Kidude
alikuwa karibu sana na Globu ya Jamii kiasi ya kwamba pamoja na umri wake
mkubwa, mara kadhaa alikuwa anatutia moyo wa kuendeleza libeneke kwa namna
ambayo haitoweza kusahaulika.
Alikuwa mtu wa karibu sana na Ankal, ambaye hata katika hali yake ya kudhoofu kutokana na umri na maradhi hakukosa kumtambua na kumtania. Ankal ni mmoja wa wanaLibeneke wachache ambao Bi Kidude aliwakubalia kupozi kupigwa picha nao.
Alikuwa mtu wa karibu sana na Ankal, ambaye hata katika hali yake ya kudhoofu kutokana na umri na maradhi hakukosa kumtambua na kumtania. Ankal ni mmoja wa wanaLibeneke wachache ambao Bi Kidude aliwakubalia kupozi kupigwa picha nao.
Ni kweli kwamba kila mtu ataonja mauti, lakini si uwongo
kwamba kuondokewa na kipenzi chetu Bi Kidude ni pigo kubwa kwa Globu ya Jamii
kama ilivyo kwa jamii yote ya tasnia ya sanaa katika Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
MOLA AIWEKA MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU BI KIDUDE
AMEN
Ankal samahani si vizuri kuuliza swali hili hapa ila naomba uniruhusu niliulize.Jina Kidude lilikuwa jina la kimuziki au ndilo haswaa jina lake halisi??Mimi nilidhani jina Kidude alilibuni mwenye kwa ajili ya shughuli zake za uimbaji kama wanavyofanya wanamuziki wengi duniani.RIP Bi Kidude
ReplyDeleteDavid V
Inashangaza sana, huyu mama mbona hakupelekwa India au SA? What is the criteria of sending Tanzanians to India? She deserved to be looked after just like any other citizen. We are sending highly paid politians and bureacrats and forgetting the poor citizens.
ReplyDeleteAnony wa pili napenda nikuulize, kwani angepelekwa india ndo indefanya asife?
ReplyDeleteShukran mtoa comment wa juu kuhusu kupelekwa nje. AGE na wakti. Alhamdulillah bibi yetu kafikia umri huo ambao ni wachache sana wataufikia. Mungu amlaze mahali pema peponi.
ReplyDeleteLakini hakuhudumiwa na wasanii wenzake kama ilivyoelezwa siku za nyuma .Leo mnamlilia..wasanii hebu tumia umoja wenu kusaidiana wakati wa haja
ReplyDeleteMdau unaetaka apelekwe India, Bi Kidude alikuwa ana miaka zaidi ya 100, anasema alizaliwa enzi za Rupia, sasa tafakuri Rupia ilitumika miaka gani, then pata jibu na ukisikia amefariki shukuru AlhamduliLLAh amefika hapo je sisi tutafika huko ? Allah ampumzishe bibi wa watu, watu wamechuma sana kwa kumpitia mwache apumzike, maana mwisho walimfanya kama katuni !
ReplyDelete