Na. ELIPHACE MARWA 
na FRANK SHIJA - MAELEZO
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akichanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar kaushiria Muungano uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka 49 iliyopita.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala Muungano Mh. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa watanzania kujitokeza kwa wingi kesho katika maadhimisho ya miaka 49 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wahabari kuzungumzia maadhimisho hayo  yatakayofanyika kesho katika uwanjwa wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa kesho ni siku muhimu kwa Watanzania kuenzi na kuudumisha Muungano kwa  kuwa umesababisha Tanzania kupata heshima kubwa Afrika na duniani kote.
 “Ninatoa wito kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya miaka 49 ya Muungano wetu, kwani hakuna asiyejua kuwa Muungano huu umetuletea heshima kubwa kimataifa, hivyo ni wajibu wetu kuulinda na kuudumisha” amesema Mh. Samia.
Aidha  Waziri huyo amesema kuwa pamoja na changamoto zilizopo Muungano umeendelea kuimarika kwa kuwa wananchi wana imani kubwa na Muungano huu na Serikali imeendelea kushughulikia kero mbalimbali za Muungano.
Mh. Samia ameongeza kuwa katika kushughukia kero zilizopo katika Muungano , Serikali ya awamu ya tatu mwaka 2004 iliunda kamati yenye wajumbe kutoka pande mbili za Muungano ya kushughulikia kero hizo.
Aidha,mwaka 2006 kamati hiyo  ilianza kushughulikia kero hizo mpaka sasa jumla ya hoja tisa kati ya hoja 13 za Muungano zimekwisha kamilika na kupatiwa ufumbuzi.
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliasisiwa na  Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Abeid Aman Karume tangu tarehe 26/04/1964  ambapo kesho unatimiza  miaka 49.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mungano mzuri halafu mikamati tele ya kurekebisha kero. Sasa kinasherehekewa nini? Kero au Muungano?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...